Benki ya Absa Tanzania imezindua rasmi Absa Lipa Sasa, huduma mpya ya malipo ya kidijitali inayotumia mfumo wa TanQR, ikiwa na lengo la kuwawezesha wafanyabiashara na watumiaji kufanya malipo kwa haraka, usalama na urahisi kupitia mfumo mmoja unaokubalika na benki mbalimbali pamoja na mitandao ya simu nchini.
Huduma hiyo imejengwa kwa kuzingatia kiwango cha kitaifa cha TanQR chini ya usimamizi wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), na inawawezesha wafanyabiashara kupokea malipo kutoka benki mbalimbali na mitandao ya simu kwa kutumia QR Code moja, hivyo kurahisisha miamala na kupunguza gharama za uendeshaji wa biashara.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mkuu wa Kitengo cha Biashara wa Benki ya Absa Tanzania, Victor Nchimbi, alisema huduma hiyo imeundwa kurahisisha malipo kwa wafanyabiashara na wateja wao.
“Kupitia Absa Lipa Sasa, mfanyabiashara anahitaji QR Code moja tu kupokea malipo kutoka kwa wateja wanaotumia benki tofauti au mitandao mbalimbali ya simu. Hii inaondoa ulazima wa kutumia vifaa au mifumo mingi ya malipo, hivyo kupunguza gharama za biashara, kuongeza kasi ya miamala, kuboresha utunzaji wa kumbukumbu na kuimarisha usalama wa malipo. Kwa wateja, huduma hii inaleta uzoefu rahisi, salama na unaotegemewa wa kufanya malipo ya kidijitali,” alisema Nchimbi.
Alieleza kuwa uzinduzi wa huduma hiyo unaunga mkono juhudi za Serikali ya Tanzania za kuongeza ujumuishaji wa huduma za kifedha na kuharakisha matumizi ya teknolojia katika shughuli za kiuchumi kupitia mifumo ya malipo ya kidijitali.
Kwa kutumia uwezo wa mfumo wa TanQR, Absa Lipa Sasa inawawezesha wafanyabiashara kupokea malipo yote kupitia mfumo mmoja bila kuwa na ulazima wa kutumia mifumo au vifaa tofauti vya malipo.
Akizungumza zaidi kuhusu faida za huduma hiyo Nchimbi alisema QR Code hiyo moja inakubali malipo kutoka benki mbalimbali na mitandao ya simu huku uthibitisho wa miamala ukipatikana papo hapo.
Aliongeza kuwa mfumo huo unapunguza utegemezi wa fedha taslimu, kuongeza uwazi katika miamala ya malipo na kupunguza gharama za kupokea malipo, hususan kwa biashara ndogo, za kati na za kati zinazokua (MSMEs).
"Huduma hiyo inalenga kuwahudumia wafanyabiashara wadogo, wa kati na wakubwa, pamoja na wafanyabiashara wa sekta isiyo rasmi wanaohitaji njia salama, rahisi na yenye ufanisi ya kupokea malipo", aliongeza.
Kwa upande wake, Meneja Masoko, Mawasiliano na Chapa wa Benki ya Absa Tanzania, Beda Biswalo, alisema uzinduzi wa Absa Lipa Sasa unaakisi dhamira ya benki hiyo ya kuwasaidia wateja kufikia malengo yao kupitia suluhisho bunifu za malipo.
“Katika Absa tunaamini kuwa ‘Stori Yako Ina Thamani’ kwa sababu kila mteja, mjasiriamali na biashara ina ndoto zinazostahili kuungwa mkono. Absa Lipa Sasa inaonesha dhamira yetu ya kuwasaidia wateja wetu kukua kupitia huduma rahisi, salama na zinazopatikana kirahisi ambazo zinakidhi mahitaji yao ya kila siku.
Hivi ndivyo tunavyotekeleza lengo letu la ‘Kuiwezesha Afrika ya Kesho, Pamoja… Hatua Moja Baada ya Nyingine,’ huku tukichochea ujumuishaji wa huduma za kifedha na mageuzi ya kidijitali nchini Tanzania,” alisema Biswalo.
Kupitia Absa Lipa Sasa, wafanyabiashara watapanua wigo wa wateja wao, kupunguza hatari zinazotokana na matumizi ya fedha taslimu, pamoja na kujenga historia ya miamala ya kidijitali ambayo inaweza kusaidia kupata huduma nyingine za kifedha siku zijazo.
Huduma hiyo ni sehemu ya mkakati mpana wa Benki ya Absa Tanzania wa kuendeleza mageuzi ya kidijitali na kuimarisha nafasi yake kama mshirika wa kuaminika wa kifedha na taasisi inayochangia maendeleo chanya ya jamii.
Absa Lipa Sasa imeanza kupatikana kwa wafanyabiashara kote nchini, ambapo usajili unaweza kufanyika katika matawi yote ya Benki ya Absa Tanzania au kupitia wasimamizi wa mahusiano ya wateja wa benki hiyo.

Mkuu wa Kitengo cha Biashara wa Benki ya Absa, Bw. Victor Nchimbi (katikati), Meneja Masoko, Mawasiliano na Chapa, Bw. Beda Biswalo ( kushoto ) na Meneja Bidhaa Kitengo cha Biashara wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Devroda Kagusa wakifanya malipo kwa simu kwa kutumia mfumo wa malipo wa Absa Lipa Sasa, wakati wa uzinduzi wa mfumo huo jijini Dar es Salaam leo. Kupitia Absa Lipa Sasa, wateja wanaweza kulipa kutoka benki au mtandao wowote kwa kutumia QR code au lipa namba hivyo kurahisisha malipo kwa kutumia njia za kidigitali.

Mkuu wa Kitengo cha Biashara wa Benki ya Absa, Bw. Victor Nchimbi (wa tano kushoto), Meneja Masoko, Mawasiliano na Chapa, Bw. Beda Biswalo (wa nne kushoto ) na Meneja Bidhaa Kitengo cha Biashara, Bi. Devroda Kagusa (wa tatu kulia), pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa benki hiyo, wakizindua mfumo wa malipo wa Absa Lipa Sasa, wakati wa mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo. Kupitia Absa Lipa Sasa, wateja wanaweza kulipa kutoka benki au mtandao wowote kwa kutumia QR code au lipa namba hivyo kurahisisha malipo kwa kutumia njia za kidigitali.
Huduma hiyo imejengwa kwa kuzingatia kiwango cha kitaifa cha TanQR chini ya usimamizi wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), na inawawezesha wafanyabiashara kupokea malipo kutoka benki mbalimbali na mitandao ya simu kwa kutumia QR Code moja, hivyo kurahisisha miamala na kupunguza gharama za uendeshaji wa biashara.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mkuu wa Kitengo cha Biashara wa Benki ya Absa Tanzania, Victor Nchimbi, alisema huduma hiyo imeundwa kurahisisha malipo kwa wafanyabiashara na wateja wao.
“Kupitia Absa Lipa Sasa, mfanyabiashara anahitaji QR Code moja tu kupokea malipo kutoka kwa wateja wanaotumia benki tofauti au mitandao mbalimbali ya simu. Hii inaondoa ulazima wa kutumia vifaa au mifumo mingi ya malipo, hivyo kupunguza gharama za biashara, kuongeza kasi ya miamala, kuboresha utunzaji wa kumbukumbu na kuimarisha usalama wa malipo. Kwa wateja, huduma hii inaleta uzoefu rahisi, salama na unaotegemewa wa kufanya malipo ya kidijitali,” alisema Nchimbi.
Alieleza kuwa uzinduzi wa huduma hiyo unaunga mkono juhudi za Serikali ya Tanzania za kuongeza ujumuishaji wa huduma za kifedha na kuharakisha matumizi ya teknolojia katika shughuli za kiuchumi kupitia mifumo ya malipo ya kidijitali.
Kwa kutumia uwezo wa mfumo wa TanQR, Absa Lipa Sasa inawawezesha wafanyabiashara kupokea malipo yote kupitia mfumo mmoja bila kuwa na ulazima wa kutumia mifumo au vifaa tofauti vya malipo.
Akizungumza zaidi kuhusu faida za huduma hiyo Nchimbi alisema QR Code hiyo moja inakubali malipo kutoka benki mbalimbali na mitandao ya simu huku uthibitisho wa miamala ukipatikana papo hapo.
Aliongeza kuwa mfumo huo unapunguza utegemezi wa fedha taslimu, kuongeza uwazi katika miamala ya malipo na kupunguza gharama za kupokea malipo, hususan kwa biashara ndogo, za kati na za kati zinazokua (MSMEs).
"Huduma hiyo inalenga kuwahudumia wafanyabiashara wadogo, wa kati na wakubwa, pamoja na wafanyabiashara wa sekta isiyo rasmi wanaohitaji njia salama, rahisi na yenye ufanisi ya kupokea malipo", aliongeza.
Kwa upande wake, Meneja Masoko, Mawasiliano na Chapa wa Benki ya Absa Tanzania, Beda Biswalo, alisema uzinduzi wa Absa Lipa Sasa unaakisi dhamira ya benki hiyo ya kuwasaidia wateja kufikia malengo yao kupitia suluhisho bunifu za malipo.
“Katika Absa tunaamini kuwa ‘Stori Yako Ina Thamani’ kwa sababu kila mteja, mjasiriamali na biashara ina ndoto zinazostahili kuungwa mkono. Absa Lipa Sasa inaonesha dhamira yetu ya kuwasaidia wateja wetu kukua kupitia huduma rahisi, salama na zinazopatikana kirahisi ambazo zinakidhi mahitaji yao ya kila siku.
Hivi ndivyo tunavyotekeleza lengo letu la ‘Kuiwezesha Afrika ya Kesho, Pamoja… Hatua Moja Baada ya Nyingine,’ huku tukichochea ujumuishaji wa huduma za kifedha na mageuzi ya kidijitali nchini Tanzania,” alisema Biswalo.
Kupitia Absa Lipa Sasa, wafanyabiashara watapanua wigo wa wateja wao, kupunguza hatari zinazotokana na matumizi ya fedha taslimu, pamoja na kujenga historia ya miamala ya kidijitali ambayo inaweza kusaidia kupata huduma nyingine za kifedha siku zijazo.
Huduma hiyo ni sehemu ya mkakati mpana wa Benki ya Absa Tanzania wa kuendeleza mageuzi ya kidijitali na kuimarisha nafasi yake kama mshirika wa kuaminika wa kifedha na taasisi inayochangia maendeleo chanya ya jamii.
Absa Lipa Sasa imeanza kupatikana kwa wafanyabiashara kote nchini, ambapo usajili unaweza kufanyika katika matawi yote ya Benki ya Absa Tanzania au kupitia wasimamizi wa mahusiano ya wateja wa benki hiyo.

Mkuu wa Kitengo cha Biashara wa Benki ya Absa, Bw. Victor Nchimbi (katikati), Meneja Masoko, Mawasiliano na Chapa, Bw. Beda Biswalo ( kushoto ) na Meneja Bidhaa Kitengo cha Biashara wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Devroda Kagusa wakifanya malipo kwa simu kwa kutumia mfumo wa malipo wa Absa Lipa Sasa, wakati wa uzinduzi wa mfumo huo jijini Dar es Salaam leo. Kupitia Absa Lipa Sasa, wateja wanaweza kulipa kutoka benki au mtandao wowote kwa kutumia QR code au lipa namba hivyo kurahisisha malipo kwa kutumia njia za kidigitali.

Mkuu wa Kitengo cha Biashara wa Benki ya Absa, Bw. Victor Nchimbi (wa tano kushoto), Meneja Masoko, Mawasiliano na Chapa, Bw. Beda Biswalo (wa nne kushoto ) na Meneja Bidhaa Kitengo cha Biashara, Bi. Devroda Kagusa (wa tatu kulia), pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa benki hiyo, wakizindua mfumo wa malipo wa Absa Lipa Sasa, wakati wa mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo. Kupitia Absa Lipa Sasa, wateja wanaweza kulipa kutoka benki au mtandao wowote kwa kutumia QR code au lipa namba hivyo kurahisisha malipo kwa kutumia njia za kidigitali.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...