Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, ameipongeza kampuni ya Yas kwa ushiriki wake katika Maonesho ya Nanenane ya Mkoa wa Lindi, akisema mchango wa sekta binafsi unaendelea kuwa nguzo muhimu katika kuharakisha maendeleo ya kilimo na mageuzi ya kidijitali nchini.
Mhe. Sangu aliyasema hayo alipotembelea Banda la Yas na kupokea maelezo kuhusu huduma za mawasiliano na kifedha kidijitali zinazotolewa na Yas na Mixx.
Kwa upande wake, Meneja wa Biashara na Masoko wa Yas - Kanda ya Pwani Kusini, Bw. George Msofe, alisema maonesho hayo yameendelea kuwa jukwaa muhimu la kuwafikia wakulima na wananchi kwa kuwaelimisha kuhusu suluhisho za kidijitali zinazorahisisha mawasiliano, malipo na ukuaji wa biashara.
"Yas itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kuhakikisha teknolojia na huduma za kidijitali zinawafikia Watanzania wengi zaidi, hususan wakulima, ili kuwawezesha kuongeza tija na kushiriki kikamilifu katika uchumi wa kidijitali," alisema Msofe.
Mhe. Sangu aliyasema hayo alipotembelea Banda la Yas na kupokea maelezo kuhusu huduma za mawasiliano na kifedha kidijitali zinazotolewa na Yas na Mixx.
Kwa upande wake, Meneja wa Biashara na Masoko wa Yas - Kanda ya Pwani Kusini, Bw. George Msofe, alisema maonesho hayo yameendelea kuwa jukwaa muhimu la kuwafikia wakulima na wananchi kwa kuwaelimisha kuhusu suluhisho za kidijitali zinazorahisisha mawasiliano, malipo na ukuaji wa biashara.
"Yas itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kuhakikisha teknolojia na huduma za kidijitali zinawafikia Watanzania wengi zaidi, hususan wakulima, ili kuwawezesha kuongeza tija na kushiriki kikamilifu katika uchumi wa kidijitali," alisema Msofe.







Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...