Waziri wa Kilimo, Mhe. Daniel Chongolo, ameiagiza Taasisi ya Kuthibiti Ubora wa Mbegu Tanzania (TOSCI) kuhakikisha inaratibu na kusimamia bei za mbegu nchini ili kuwawezesha wakulima kupata taarifa sahihi za bei na kununua mbegu bora kwa bei zinazozingatia taratibu zilizowekwa.
Chongolo ametoa agizo hilo leo jijini Dar es Salaam wakati wa kikao cha wadau wa tasnia ya mbegu akisema mbegu ni miongoni mwa pembejeo muhimu katika uzalishaji wa mazao, hivyo kuna umuhimu wa kuwepo kwa mfumo utakaomwezesha mkulima kufahamu bei ya mbegu kabla ya kufanya manunuzi.
Amesema TOSCI, kwa nafasi yake ya kusimamia ubora wa mbegu nchini, inapaswa pia kuhakikisha kampuni zia mbegu zinasambaza na kuuza mbegu kwa ushindani kwa bei ambazo TOSCI itazisimamia.
“Tumekuwa na utaratibu kwenye mbolea ambapo TFRA ndiyo inayoratibu na kusimamia bei za mbolea”. Mbegu nazo ni pembejeo za kilimo, hivyo hapa TOSCI ina wajibu wa kuratibu,” amesema Mheshimiwa Chongolo.
Aidha, amezitaka kampuni za mbegu kuhakikisha mbegu bora zinawafikia wakulima kwa wakati kupitia mawakala wanaokidhi vigezo, huku akisisitiza umuhimu wa kuongeza uzalishaji wa mbegu nchini. Amesema Tanzania ina ardhi na mazingira bora yanayowezesha kuongeza uzalishaji wa mbegu ndani ya nchi na hivyo kupunguza utegemezi wa mbegu kutoka nje ya nchi.




.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...