-Apanga kuitisha kikao cha wasafirishaji wa mizigo
-Aomba wakulima watumie mbolea zinazozalishwa nchini
WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amesema kuanza uzalishaji kwa kiwanda cha saruji cha Kigoma kutasaidia kuondoa tatizo la kupanda bei kwa bidhaa hiyo kwenye mikoa ya Magharibi mwa Tanzania.
Amesema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amesisitiza katika dira yake ya uwekezaji kwamba kuwe na viwanda katika kanda mbalimbali za nchi ili kupunguza changamoto za gharama za usafirishaji. “Pale gharama za usafirishaji zinapopanda, bei ya bidhaa nayo hupanda,” amesema.
Ametoa kauli hiyo Bungeni jijini Dodoma, leo (Alhamisi, Septemba 03, 2026) wakati akijibu swali la Mbunge wa Kasulu Vijijini, Bw. Edibily Kazala Kinyoma, kwenye kipindi cha maswali ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu ambaye alitaka kujua kauli ya Serikali kuhusu kuanzisha tathmini ya gharama halisi za uzalishaji wa saruji nchini ili kuwe na bei elekezi itakayotoa unafuu kwa wananchi na kuchochea sekta ya ujenzi Tanzania.
Mbunge huyo amesema pamoja na uwekezaji uliofanyika kwenye sekta ya viwanda, bado kuna changamoto katika upande wa saruji kwani bei yake imekuwa ikipanda kwa kasi na baadhi ya maeneo imefikia zaidi ya sh. 25,000.
“Habari njema ni kwamba Mheshimiwa Rais tayari ameelekeza watu wanaotaka kuwekeza katika bidhaa hizi wapewe kipaumbele. Kwa taarifa nilizonazo, kule Kigoma kuna kiwanda kimojawapo cha saruji ambacho kiko katika hatua za utekelezaji. Lengo ni kuwa na viwanda vingine vinavyozalisha bidhaa hii katika maeneo ya magharibi mwa nchi ikiwemo Kigoma, Kagera na Katavi,” amesema.
Dkt. Mwigulu amesema kuwepo kwa viwanda kama hivyo kwenye mikoa na kanda tofauti kutasaidia kupunguza gharama za kusafirisha saruji kutoka Mtwara au Tanga kwenda upande mwingine wa nchi, jambo ambalo linaongeza gharama za usafirishaji na usambazaji.
Amesema amepanga kuitisha kikao kitakachowahusisha wasambazaji mbalimbali nchini ili kujadiliana nao namna ya kudhibiti ongezeko la bei na kuhakikisha wananchi hawaathiriki kwa kiwango kikubwa, jambo ambalo anaamini litasaidia kupunguza gharama za ujenzi na kuchochea maendeleo.
“Jambo hili la bei ya saruji linagusa maisha ya kila Mtanzania na kupanda kwa bei ya saruji hivi karibuni kumehusishwa pia na kupanda kwa bei za mafuta, jambo ambalo limeongeza gharama za usafirishaji. Serikali imeshakaa na wadau wa usafirishaji na kutafuta namna ya kupunguza gharama hizo. Nimekwishakutana na wasafirishaji wa abiria, na nimepanga pia kukutana na wasafirishaji wa mizigo ili kuangalia maeneo tunayoweza kuyarekebisha na kupunguza gharama za usafirishaji,” amesema.
Katika hatua nyingine, akijibu swali kuhusu upatikanaji wa mbolea, Waziri Mkuu amesema Serikali imechukua hatua za muda wa kati kwa kukaa na waagizaji wa mbolea na kuwaelekeza waangalie uwezekano wa kuagiza bidhaa hiyo kutoka nchi mbadala badala ya kutegemea nchi za Ulaya Mashariki.
“Tumefanya hivyo pia kwa bidhaa nyingine, ikiwemo sukari. Kwa upande wa mbolea, tumeagiza kutoka nchi za Afrika, ikiwemo Morocco, na pia kuwaelekeza waagizaji waangalie masoko ya China ili kuhakikisha bidhaa hizo zinakuwepo nchini,” amesema.
Alikuwa akijibu swali la Mbunge Momba, Bi. Condester Sichalwe aliyetaka kujua Serikali imejipangaje kuhakikisha mbolea za ruzuku na pembejeo nyingine zinazolenga kumfanya mkulima kuwa mwekezaji na kilimo kuwa biashara zinafika kwa wakati na kuleta tija.
Dkt. Mwigulu amesema ili kupunguza utegemezi wa bidhaa kutoka nje na kuepuka matatizo ya usafirishaji, kwa muda mrefu, Serikali imeendelea kuhamasisha uwekezaji katika viwanda vya kuzalisha mbolea hapa nchini.
“Kiwanda kilichopo Dodoma kimeanza kufanya kazi. Pia tunaendelea kuhamasisha wakulima kutumia mbolea zinazozalishwa nchini, ikiwemo mbolea ya Mijingu kutoka Arusha, ambayo inatumika kwa kiwango kikubwa katika nchi jirani kuliko hapa Tanzania. Tunaendelea pia kuhamasisha viwanda vingine, hasa vile vinavyozalisha aina muhimu za mbolea ambazo tumekuwa tukiziagiza kutoka nje.”
Amesema Serikali imeendelea kuwalipa waagizaji wa mbolea ili kuhakikisha wanakuwa na ukwasi wa kutosha wa kuagiza mbolea na pembejeo nyingine kwa wakati. Wakati huohuo, tunazihimiza taasisi zinazosimamia usambazaji wa mbolea na sekta hiyo kufanya kazi kwa wakati. “Misimu ya kilimo siyo ya dharura, inajulikana mkoa gani unaanza msimu wa kilimo lini. Kwa hiyo, tunapaswa kupanga mapema ili mbolea na pembejeo ziwepo kabla ya msimu kuanza,” amesisitiza.
-Aomba wakulima watumie mbolea zinazozalishwa nchini
WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amesema kuanza uzalishaji kwa kiwanda cha saruji cha Kigoma kutasaidia kuondoa tatizo la kupanda bei kwa bidhaa hiyo kwenye mikoa ya Magharibi mwa Tanzania.
Amesema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amesisitiza katika dira yake ya uwekezaji kwamba kuwe na viwanda katika kanda mbalimbali za nchi ili kupunguza changamoto za gharama za usafirishaji. “Pale gharama za usafirishaji zinapopanda, bei ya bidhaa nayo hupanda,” amesema.
Ametoa kauli hiyo Bungeni jijini Dodoma, leo (Alhamisi, Septemba 03, 2026) wakati akijibu swali la Mbunge wa Kasulu Vijijini, Bw. Edibily Kazala Kinyoma, kwenye kipindi cha maswali ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu ambaye alitaka kujua kauli ya Serikali kuhusu kuanzisha tathmini ya gharama halisi za uzalishaji wa saruji nchini ili kuwe na bei elekezi itakayotoa unafuu kwa wananchi na kuchochea sekta ya ujenzi Tanzania.
Mbunge huyo amesema pamoja na uwekezaji uliofanyika kwenye sekta ya viwanda, bado kuna changamoto katika upande wa saruji kwani bei yake imekuwa ikipanda kwa kasi na baadhi ya maeneo imefikia zaidi ya sh. 25,000.
“Habari njema ni kwamba Mheshimiwa Rais tayari ameelekeza watu wanaotaka kuwekeza katika bidhaa hizi wapewe kipaumbele. Kwa taarifa nilizonazo, kule Kigoma kuna kiwanda kimojawapo cha saruji ambacho kiko katika hatua za utekelezaji. Lengo ni kuwa na viwanda vingine vinavyozalisha bidhaa hii katika maeneo ya magharibi mwa nchi ikiwemo Kigoma, Kagera na Katavi,” amesema.
Dkt. Mwigulu amesema kuwepo kwa viwanda kama hivyo kwenye mikoa na kanda tofauti kutasaidia kupunguza gharama za kusafirisha saruji kutoka Mtwara au Tanga kwenda upande mwingine wa nchi, jambo ambalo linaongeza gharama za usafirishaji na usambazaji.
Amesema amepanga kuitisha kikao kitakachowahusisha wasambazaji mbalimbali nchini ili kujadiliana nao namna ya kudhibiti ongezeko la bei na kuhakikisha wananchi hawaathiriki kwa kiwango kikubwa, jambo ambalo anaamini litasaidia kupunguza gharama za ujenzi na kuchochea maendeleo.
“Jambo hili la bei ya saruji linagusa maisha ya kila Mtanzania na kupanda kwa bei ya saruji hivi karibuni kumehusishwa pia na kupanda kwa bei za mafuta, jambo ambalo limeongeza gharama za usafirishaji. Serikali imeshakaa na wadau wa usafirishaji na kutafuta namna ya kupunguza gharama hizo. Nimekwishakutana na wasafirishaji wa abiria, na nimepanga pia kukutana na wasafirishaji wa mizigo ili kuangalia maeneo tunayoweza kuyarekebisha na kupunguza gharama za usafirishaji,” amesema.
Katika hatua nyingine, akijibu swali kuhusu upatikanaji wa mbolea, Waziri Mkuu amesema Serikali imechukua hatua za muda wa kati kwa kukaa na waagizaji wa mbolea na kuwaelekeza waangalie uwezekano wa kuagiza bidhaa hiyo kutoka nchi mbadala badala ya kutegemea nchi za Ulaya Mashariki.
“Tumefanya hivyo pia kwa bidhaa nyingine, ikiwemo sukari. Kwa upande wa mbolea, tumeagiza kutoka nchi za Afrika, ikiwemo Morocco, na pia kuwaelekeza waagizaji waangalie masoko ya China ili kuhakikisha bidhaa hizo zinakuwepo nchini,” amesema.
Alikuwa akijibu swali la Mbunge Momba, Bi. Condester Sichalwe aliyetaka kujua Serikali imejipangaje kuhakikisha mbolea za ruzuku na pembejeo nyingine zinazolenga kumfanya mkulima kuwa mwekezaji na kilimo kuwa biashara zinafika kwa wakati na kuleta tija.
Dkt. Mwigulu amesema ili kupunguza utegemezi wa bidhaa kutoka nje na kuepuka matatizo ya usafirishaji, kwa muda mrefu, Serikali imeendelea kuhamasisha uwekezaji katika viwanda vya kuzalisha mbolea hapa nchini.
“Kiwanda kilichopo Dodoma kimeanza kufanya kazi. Pia tunaendelea kuhamasisha wakulima kutumia mbolea zinazozalishwa nchini, ikiwemo mbolea ya Mijingu kutoka Arusha, ambayo inatumika kwa kiwango kikubwa katika nchi jirani kuliko hapa Tanzania. Tunaendelea pia kuhamasisha viwanda vingine, hasa vile vinavyozalisha aina muhimu za mbolea ambazo tumekuwa tukiziagiza kutoka nje.”
Amesema Serikali imeendelea kuwalipa waagizaji wa mbolea ili kuhakikisha wanakuwa na ukwasi wa kutosha wa kuagiza mbolea na pembejeo nyingine kwa wakati. Wakati huohuo, tunazihimiza taasisi zinazosimamia usambazaji wa mbolea na sekta hiyo kufanya kazi kwa wakati. “Misimu ya kilimo siyo ya dharura, inajulikana mkoa gani unaanza msimu wa kilimo lini. Kwa hiyo, tunapaswa kupanga mapema ili mbolea na pembejeo ziwepo kabla ya msimu kuanza,” amesisitiza.


.jpeg)


.jpeg)


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...