
jk akilakiwa na wabongo kibao waliofika uwanja wa ndege wa sitokihomu usiku wa leo akiwa tayari kuanza ziara yake ya nchi za unordiki akianzia uswidi. nyeti zinadatisha kwamba wabongo wengi sana walifika eapoti kumpokea na wengi zaidi walikuwepo kwenye mkia wa jogoo waliomwandalia kwenye hoteli alofikia ambako aliongea nao kwa muda. mengi zaidi baadaye, stei tyuundi


JK ANAPOWANYESHEA BUSARA NA HEKIMA WAKIMBIZI KUTOKA TANZANIA
ReplyDelete“ Kama kuna anayejiita mkimbizi bila shaka aliingia hapa akiwa na pasipoti ya Tanzania, na kama alipanda ndege hakuna ndege utakayopanda bila kuonyesha pasipoti, sasa nataka nipate ufafanuzi tatizo liko wapi, kama pasi imekwisha muda wake basi si aende tu akaongezewe muda ” akahoji rais Kikwete.
Na kuongeza “ Kama kuna mtu aliyeikana Tanzania akasema nchi gani ile hata kuishi haifai mimi nataka kuishi hapa (London), kama kuna mtu aliichana pasipoti yake, akaiponda Tanzania, ‘akajilipua’ sasa ametubu kwamba amekosa anataka apewe pasi yake ya Tanzania naye atueleze hapa ili na mimi nijue nianzie wapi,” alifafanua rais Kikwete kwa ithibati ya hali ya juu.
HAKUNA MDAU ALIYEJITOKEZA MPAKA TUNAINGIA MITAMBONI
Michuzi nawasilisha hoja kwamba wasaliti hawana nafasi katika taifa la Tanzania.Hawa wakija watauza nchi yetu, bora wanasiasa wetu wa sasa tushawazoea na longo longo zao.
Ha ha ha ha ha
ReplyDeleteMichuzi, ama unaanza kuvumbua lugha yako sasa, nimejiuliza , huu mkia wa jogoo ndo mdudu gani. La haula, kumbe ni COCKTAIL. Ha ha ha ha ha ha
Yaani nimecheka sana kugundua kuwa Mkia wa jogoo ni cocktail.
Asante umenipa msamiati mpya kaka
Ni hayo tu
nadhani wakati umefika sasa kwa watu kuipenda nchi yao. ukichana paspoti kama mkimbizi wakati nchini hakuna vita ni hatari. vijana wapige goti tu watasamehewa lakini walikosea
ReplyDeleteHII KALI JAMANIIIIIIII.....
ReplyDeletehttp://bp2.blogger.com/_stxylFr6jLM/RdNx44a2MYI/AAAAAAAABN8/KvoNLLvdDQ0/s1600-h/STA70161.JPG
hhahahahahah nakuunga mkono hapo juu hata mie sikujua anamaanisha nini hadi nimesoma post yako ndio nimegundua > Michuzi anafurahisha sana na misamiati yake mara ukerewe nakadhali huwaga napitia humu kupata vichekesho ama hivyo Big up Michuzi hahahaahah cocktail LOL
ReplyDeletehapo walijaa wakimbizi tu wengi wasomali na waburundi
ReplyDeleteSitoki HOME sio!
ReplyDeleteTatizo ndio hilo, raisi anataka watu warudi nyumbani badala ya ku-encourage watu wawavute wenzao wengi ili wasaidie nyumbani (kusaidia pia uchumi kwa kutuma fedha za kigeni nyumbani)yeye anataka tugawane umaskini!!!Hajui kuwa wawekezaji ndio wanaohamisha madola yetu kwani hawaweki pesa zao kwenye mabenki yetu na kufanya dola kuhadimika hivyo kuwa juu.
ReplyDeleteWatanzania mlioko nje mnaweza kuwa wazalendo wa nchi mkiwa huko huko kwa kuanzisha makampuni na maduka ya biashara ya bidhaa za Tanzania.
ReplyDeleteWahindi,waarabu na wachina ni mfano mzuri wa watu wazalendo wa nchi zao, wawapo katika nchi zingine.
Mfano Wahindi walioko Tanzania ndio wafanyabiashara wakubwa wa bidhaa zitokazo na kwenda India nchini Tanzania,Pia waarabu walioko Tanzania ndio wafanya biashara wakubwa wa Bidhaa toka Uarabuni kama mafuta,vipuri ,magari toka dubai n.k na pia ndio wapelekaji uarabuni bidhaa zitokazo Tanzania,Wachina pia walioko Tanzania ndio wafanyabiashara wakuu wa bidhaa za China kuanzia dawa za kienyeji,Bidhaa za viwandani n.k.
Ni wakati wenu kuanza kuwa wafanyabiashara wa bidhaa za Tanzania huko.Unganeni muwe na mitaji mikubwa na muanze kuuza bidhaa za Tanzania huko.
Msikubali tu kuwa promoters mnaotafuta watu tu wa kuja kuchukua bidhaa huku njooni mchukue wenyewe muwauzie huko. Ingiine kwenye biashara.Hata makampuni ya kuleta watalii mnaweza anzisha huko nje ya nchi, hata mkaingia ubia na wenyeji wa huko mkapata faida kubwa.
Nawatakia kila la heri.
koloboi@yahoo.com