Mr Michuzi nashukuru sana kwa kutupatia taarifa muhimu katika hii blog yako. Sasa mie ni mkazi wa Arusha (A Town) tangu juzi kuna matetemeko ya ardhi yanapita na yanatikisa vibaya sana. Usiku sikulala kwan kitanda kilikua kinatingishika kama mtu yupo uvunguni anakitikisa!!
Tunaomba wataalamu wa hali ya hewa watueleze kiufasaha kuhusu hali hii ili tujihami mapema!!
Nawasilisha
Mdau

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 14 mpaka sasa

  1. Michuzi,

    Nitakupigia simu. You sould at least make a cameo in Bongoland!

    ReplyDelete
  2. Limepita lingine sasa hivi kwenye saa kumi na moja na nusu hili limekuwa kubwa zaidi na limedum kwa muda mrefu zaidi, nadhani wa kwenye majengo marefu watakuwa wametimua mbio

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 16, 2007

    hata moja limepita sasa hivi hap ofisini tulikuwa tunachezeshwa sindimba.

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 16, 2007

    Hii issue sio utani, ni kweli. nimeongea na cousin wangu ambae yuko huko TZ, Arusha na ameniambia kuwa hata leo alikuwa ofisini akakuta Meza na samani nyingine zinatikisika.

    ni Vyema hali ya hewa watoe maelezo mapema kwani arusha kuna milima ya volcano na inawezekana volcano inajikusanya huko chini kabla ya kulipuka.

    hii ni hatari ambayo serikali isiifanyie mzaha kama ilivyofanya kwenye RVF.

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 16, 2007

    Kufuatana na habari zinazopatikana hapa Amerika, the epicentre (kitovu) cha matetemeko hayo ni kati ya TZ na DRC (Ziwa tanganyika...sana sana katika mji wa kalemea nchini DCR).

    Kuna matetemeko ya aina mbili. Moja, msuguano wa kuta za aridhi. Hii inasababisha mujengeka kwa milima. Mbili, kutengana kwa kuta za aridhi na kuleteleza kuzama kwa aridhi mabonde ya ufa.

    Matetemeko yanayotokea, na mengine ni afterquakes, ni ya aina ya pili.

    ReplyDelete
  6. AnonymousJuly 17, 2007

    Yesu, sasa kama volcano ndio inaikusanya, mboni itakuwa hatari. Maskini bibi yangu.

    ReplyDelete
  7. AnonymousJuly 17, 2007

    Labda ni aftershock ya hilo kubwa lilotokea Japani leo. Nimeona kwenye News Lao kiboko

    ReplyDelete
  8. AnonymousJuly 17, 2007

    MICHUZI TAFADHALI TUWAKILISHIE SUALA HILI KWENYE KITENGO CHA UCHUNGUZI WA HALI YA HEWA TANZANIA, ILI TUJUE KINACHOENDELEA, TUNA NDUGU ZETU ARUSHA HIVYO KAMA KUNA CHA KUFANYA ILI KUJIHAMI TUJULISHE ILI TUWASILIANE NAO MAPEMA! TUJUMUIKE KULIANGALIA SUALA HILI SERIOUSLY!! ASANTE.

    ReplyDelete
  9. AnonymousJuly 17, 2007

    Michuzi,
    Hawa jamaa wanaotoa comments huku,inabidi kuwa nao makini, Haya sasa click mwenyewe hicho ki Link cha huyo jamaa anaeitwa NGONO!!!
    Tehetehetehe!!!

    ReplyDelete
  10. AnonymousJuly 17, 2007

    Hiyo earth quake ya jana ilikuwa na magnitude 4.7, kwa habari zaidi checki - http://earthquake.usgs.gov/eqcenter/recenteqsww/Quakes/us2007ewbe.php

    ReplyDelete
  11. AnonymousJuly 17, 2007

    Update: Limepita Lingine sasa hivi tena, Haloo leo watu wametimua kutoka maofisini, nadhani hili linaweza kuwa lina build up kuja kuleta madhara makubwa siku za usoni.

    ReplyDelete
  12. AnonymousJuly 17, 2007

    MR MICHUZI, THIS IS SERIOUS MATETEMEKO BADO YAPO YANAENDELEA.. TUNAOMBA IDARA HUSIKA WATOE SABABU ZA HALI HII NA JINSI YA KUJIEPUSHA KWAN HII MITIKISIKO NI MIKUBWA BA HIZI NYUMBA ZETU ZA MBAVU ZA MBWA MTU UNAWEZA KUFA KIBUDU.

    ReplyDelete
  13. AnonymousJuly 17, 2007

    Michuzi:

    Hao wenye majina katika rangi za bluu (au majina yanayopigiwa mistari), maana yake ni kwamba ukibofya kwenye hayo majina, ni "links"; unapelekwa moja kwa moja kwenye websites zao.

    Sio wote; website nyingine ni za mambo ya ngono, kama jina la "ngono" lilivyo hapo juu!!!!!!!!

    ReplyDelete
  14. AnonymousJuly 17, 2007

    Michuzi:

    Kama alivyotahadarisha anon wa July 17, 2007 2:24:00 AM EAT, majina yenye kuandikwa kwa rangi ya bluu (au yaliyoandikwa kwa rangi nyeusi na kupigiwa mistari), ni "links" zinazokupeleka moja kwa moja kwenye websites zao, kama ukiyabofya!

    Sio wote; lakini "websites" hizi nyingine ni mazizi ya ngono, kama ilivyo kwa huyo "ngono" hapo juu!

    Websites nyingine ni mazizi ya virusi, digitally!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...