ukiingia uchagani ile pyeeee... mbege
edwin elifuraha samwel mrema na mai waifu wake mariana mtibagiligwa wakimeremeta leo baada ya kufunga ndoa kanisa la azania front na baadaye kwenye bonge la pati hoteli 92, sinza, dar

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 17 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 11, 2008

    Hongera...ngondi....nakutakia maisha mema na mwenzio....tc.

    ur mate @cs.udsm.

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 11, 2008

    hongera Ed!!!...nakutakia maisha mema..hongera sana!!!...duu nimekosa mnuso tena kama kawaida..

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 11, 2008

    Nafikiri kila kitu hufanzwa kufunza. Eti!

    Tumeaswa mara nyingi kudumisha mila na tamaduni zetu ikiwemo lugha, milo, mavazi, nyimbo n.k. Mfano humu kijijini watu wamepiga kelele ..tumieni kiswahili, acheni kiingereza... Kata aliloshika maiwaifu wa Ngondi ni la asili. Je, wadau, hilo kata la mbege na chupa ya bia kipi zaidi?

    Wasalaam,

    Seve

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 11, 2008

    Kuna utamaduni wa kutoa maelezo yanayohusiana na shughuli wazifanyazo wanandoa katika matangazo kama haya.. kwa mfano.. Bwana harusi ni mkulima na muuzaji wa viazi vitamu pale bonde la msimbazi na bibi harusi ni mshauri wa mambo ya kindoa na anamiliki saluni ya kike Sharifu shamba.

    Misupu upo hapo?

    Ignorant, Jeremani

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 11, 2008

    Hongera Edwin,
    unakumbuka huu wimbo?
    mai mongo, aichu mpora
    ende wari, na kipata

    koicho tiro tiro tiro X3
    wamrema wakupaya.

    Chamecha Mrema. Duo kiombuho arawa.
    Congratulations Edwin

    H. Mchau

    ReplyDelete
  6. AnonymousMay 11, 2008

    HUO UMBEA SASA WEWE UNATAKA KUJUA WANAFANYA KAZI GANI WA NINI WAKATI UWAJUI WAACHE WANAO WAJUA

    ReplyDelete
  7. AnonymousMay 11, 2008

    Inaelekea we annon wa 1:56 haufahamu maana ya umbea. Kufahamu kazi/shughuli ya mtu si umbea. Pia fahamu kwamba kazi imetumika kama mfano tu wa taarifa tunazoweza pewa kuwahusu hao wanaharusi.

    Naomba nipingane nawe katika msemo wako "waache wanao wajua". Nasikitika kusema kua huu ni ubinafsi na uchoyo, kwa mtazamo wangu naamini kabisa taarifa zinazotolewa hapa zinapaswa kutufaidisha wote bila kujali rangi, umri, jinsia, kabila wala ufuasi wa chama.

    Shughuli/kazi ya mtu ni moja ya taarifa za kibinafsi ambazo hazipaswi kua siri hasa kama kazi uifanyayo sio ya wizi. Hii inaweza kua mojawapo ya kupunguza mafisadi hapo bongo.

    Ngoja nikupe mfano wa jinsi unaweza kufaidika na ufahamu wa kujua shughuli/kazi ya mtu. Napenda pia kukufahamisha kua kufahamu kazi ya mtu inasaidia kuzitangaza baadhi ya kazi ambazo kwa kwetu hapo haziko vichwani mwa watu. Mtoto anakua anajua kazi ya unesi, daktari, mwalimu na pengine mwanasheria tu. Anakuja kua mtu mzima na kulaumu kwanini hakupata ufahamu wa kazi zingine ambazo pengine anadhani kwake zingekua ndiyo pendekezo.

    Jamani tujaribu kua na mawazo "positive" pindi tunaposoma maoni ya hapa kibarazani. Kuna mwingine angelilia kazi yake itangazwe ili iwe kama njia ya kujitangaza kibiashara.

    Ignorant, Jeremani

    ReplyDelete
  8. Hongera Edwin na Mariana! Mnameremeta kweli. Nawatakia maisha mema ya ndoa.

    ReplyDelete
  9. AnonymousMay 11, 2008

    Ignorant jeremani wewe ndio wale walavichwa nini mbona unataka kujua kazi za wao maharusi kwa sana kweli ni umbea kama alivyosema Anon hapo juu mbona sisi hatuja kuuliza hapo German unabeba box au uko kwenye retirement homes umeshaambiwa ni maharusi basi kazi yao ni mke na mume ok...

    ReplyDelete
  10. AnonymousMay 11, 2008

    nakuunga mkono na mguu ignorant-jeremani, hapo umesema kweli kuhusu kujua kazi,ni kweli kabisa kuna watu wakionekana wanameremeta na kazi yake ikatangazwa kuwa ni mpalamiwa[yaani anayemenya miwa] inampa moyo hata mwingine aliyekuwa anadharau kazi hiyo akidhani haiwezi kufanya life likasogea ilimradi tu aiheshimu na kuinya iwe nzuri, imean not necessary to find a good job, but we can make a job good.
    maana mitazamo ya kujuwa tu kuwa kazifulani ndio mambo safi,wengine imetufikisha mahali tunajuta na direction tulizochukuwa kwakuwa tu tulijuwa kazi ndizo hizo!
    TANGAZENI KAZI HATAKAMA YA KUZIBUA MABOMBA YA CHOO,CHAMUHIMU UNAIFANYA VIZURI NA INAKUTUNZA! maana what you are doing now is very important to you now than what you could do!
    BIG UP jeremani.

    mdau-ughaibuni

    ReplyDelete
  11. AnonymousMay 12, 2008

    huku majuu sisi wabeba box tushazoea kupewa hizo information, anafanya kazi wapi na kama nani, alisoma wapi, alisomea nini etc. for those who read "JET" magazine correct me if i am wrong!

    ReplyDelete
  12. AnonymousMay 12, 2008

    Edwin aka Epare(tuliosoma naye mlimani ndivyo tulimwita)

    Ebwana nimekubali mzee, Hongera sana kwa hatua hii muhimu ya maisha. Nakutakia kila la kheri katika maisha haya mapya uliyoyaanza. Baraka za Mwenyezi Mungu zikae juu yenu.

    Tuko nyuma tunafuata nyayo.

    Mdau Dommy Mosha aka Big Do

    ReplyDelete
  13. AnonymousMay 12, 2008

    shimboni shafo naona umekumbatia bonge la nanihiii unakunywa mwenyewe. hongereni sana mmependeza na Mungu awasaidie.
    sweet
    Arusha.

    ReplyDelete
  14. AnonymousMay 12, 2008

    Seve mengi ya kudumishwa yapo na ya kuachwa pia yapo m.f hapo kabebwa na mumewe mila zetu nyengine hapo anabebwa na bibi almaarufu KUNGWI,yuhuuuu... hapo nikikuuliza nani zaidi jibu unalo upo apo? yeeeeba!!

    ReplyDelete
  15. AnonymousMay 12, 2008

    Hongereni maharusi na ahsanteni kwa kusare nasi picha zenu. Kwa kweli kkabsa haa si mafisadi wala watoto wa mafsadi. Mnataka kujua nini zaidi? Mke ana degree 3 na ni mama wa nyumbani na mme ana degee 4 na amejiajiri mwenyewe. Hivi kuna haja ya kujua yote haya? ni utamaduni kutangaza kuwa unafanya kazi Sheraton kama mhasibu au mpishi?

    ReplyDelete
  16. AnonymousMay 12, 2008

    ignorant wa jeremani hana hoja ya nguvu,asitumie efforts nyingi kutetea position yake. Eti watoto wanahitaji kujua kuna kazi za aina gani kupitia pich ya waliofunga pingu za maisha, nenda vault.com wetfeet.com
    ask.com,google.com careerbuilders.com

    ReplyDelete
  17. AnonymousMay 14, 2008

    aah! kibarua sugu naona umevuka!!

    godfrey malunda

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...