Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 08, 2008

    Hapana, ni ile hadithi ya ndege korongo (crane) na sungura kwenye hadithi za Esopo! Korongo ana mdomo mrefu kama kaufito ka mwanzi, na huwa anafyonza vyakula vyake matopeni, hawezi kula kutoka kwenye sahani maana shurti atumbukize mdomo (beak, sijui kiswahili yake) ndipo afyonze. Sasa sungura akamwalika korongo kwenye karamu akamwekea uji kwenye sahani bapa (flat)! Basi kamkaribisha kinafiki, "karibu rafiki yangu tule pamoja"! Katika kula huko, sungura analamba uji kwenye sahani bila tatizo, ndio namna yake ya kula, lakini yeye korongo anajaribu kufyonza bila mafanikio, anaishia tu kuchafua kamdomo kake, hakumeza hata tone moja la uji! Ndiyo haya haya ya mabenki yetu na mikopo ambayo izi noti richabo!

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 08, 2008

    Kilichopo hapa ni 'conflict of interest'. Wenye mabenki wanataka faida, maana nao wako kazini, wakati mkopaji angefurahi sana kama ama angepewa mkopo usio na riba au riba iwe ndogo sana! Hapo ndiyo kwenye tatizo!

    Lakini kuna tatizo lingine kubwa hapa: Wabongo wengi wakikopa wanakwenda kufanyia 'party' badala ya shughuli ya kujiongezea kipato.

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 09, 2008

    Aliyekuambia nchi hii tuna Benki nani?Benki zinazo subiri zifuatwe na watu lakini siyo zinazo tafuta na kuwafuata wateja mahali pao pa kazi!Hazikopeshi kwa hiari bali kwa kushinikizwa.Msipokopa hiari yenu,mifedha yote itawekezwa katika Dhamana za Serikali(Treasury Bills and Government Bonds)na Benki bado itapata Faida kubwa mwisho wa mwaka kwa 'Tija na Ufanisi wa shughuli zake'.Isitoshe,katika nchi hii bwana Mikopo yote ni 'hatari'tupu,imejaa 'RISKS'Kibao!Ndiyo maana hatutoi mikopo katika sekta ya Madini wala Ujenzi.Haina dhamana!(collateral)!Kilimo nacho ardhi haijabinafsishwa sasa unafikiri nini?Utakopeshaje?Viwanda?aah,viwanda havilipi si ubora uagize bidhaa toka nchi za nje?Bei nafuu kuliko gharama ya uzalishaji hapa nchini!Uchumi kukua?aaah,uchumi utakua tu,kwani nini,si suala la kucheza na takwimu tu,sasa kumbe je?Huyo wa kuanza kupekua takwimu sekta kwa sekta na mradi kwa mradi ,mkoa kwa mkoa na wizara kwa wizara ATOKE WAPI?Mwakyembe mwenyewe kazi hiyo haiwezi!Pesa yako mwenyewe hebu kaiweke Benki uone Riba utakayo lipwa mwisho wa mwaka.Pesa yako hiyo hiyo jaribu kwenda Benki ukaikope uone Riba kiasi gani watakutoza kwa kukopa?Very Risky kukopesha Mze si unajua?Riba za Mabenki na Inflation Rate vitu mbalimbali!Unacheza na Benki za Kibongo nini?Kasi Mpya economic monetary policy!

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 10, 2008

    MHESHIMIWA WA Tarehe May 09, 2008 11:42 AM,UMEWEKA MAMBO "..BAYANA.."..SAFI SANA..WENZETU BONGO WANABEBESHWA MIKOPO AMBAYO INA INTEREST KUBWA SANA KUTOKANA NA..".. HIGH RISK..".."..INASABABISHWA NA SYSTEM MBOVU YA "..SIRIKALI.."..WALE WENYE NYUMBA AS.."..COLLATERAL.."..ZITAISHIA KUPIGWA MNADA KWASABABU HAKUNA UWIANO/UDHIBITI WA INTEREST.."..KATI YA MKOPAJI..MKOPESHAJI..NA SIRIKALI(HALI YA UCHUMI KWA UJUMLA).."..TATIZO SIO DENI.."..TATIZO NI..JE DENI LITALIPIKA..?..KIVIPI..KWA MUDA GANI..?.."..SIRIKALI NI.."..LAZIMA.."..IDHIBITI..INTEREST.."..ILI WALALA HOI WAWEZE KUKOPA NA KULIPA.."..MNAWABEBESHA WALALA HOI INTEREST .."..ZA UFISADI WENU.."..HUU UFISADI LAZIMA UFANYIWE KAZI.."

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 10, 2008

    NAKUBALIANA NA WACHANGIAJI WOTE HAPO JUU.ILA BADO KUNA TATIZO KWA WAAJIRAIWA WA MABENKI YA BOGO HASA WA LONI DIPATIMENT.NI WAVIVU SANA SANA WA KUANALAIZ RISKI! HATA KAMA BIASHARA UKI-PRROSPEKTI INALIPA VIZURI IN NEAR FIUCHA,WAO WAMEKARIRI COLATERO TU!
    HALAFU BIASHARA IKIPIKI WAO NDO WA KWANZA KUKUAMBIA NJOO U-BENKI NA SISI! WANANIUZI MMMMNOOO!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...