Mpeli Nsekela 'Kiongozi', ambaye ni meneja wa kilaji cha Ndovu Special Malt kinachotengenezwa na Tanzania Breweries Limited, akizungumzia udhamini wa kilaji hicho kwa kongamano ya utawala ifanyikayo kila mwezi katika ukumbi wa British Council jijini Dar
ALICHOKISEMA MPELI NSEKELA 'KIONGOZI' KUHUSU UDHAMINI WA NDOVU SPECIAL MALT WA MANAGEMENT FORUM IFANYIKAYO BRITISH COUNCIL, DAR, LEO:
"Ndovu Special Malt ina mwaka na zaidi tangu izinduliwe na toka izinduliwe imekuwa ikitangazwa kama Chaguo Makini kwa watu anaojua wanachokitaka katika maisha.
"Ndovu Special Malt ina furaha na heshima ya kutangaza kujumuika na British Council kufanikisha vikao vya kila mwezi vifanyikavyo hapa British Council vijulikanavyo kama Management Forum.
"Ushirikiano huu ni wa udhamini na unaanza mwezi huu wa 6 na utadumu mpaka mwaka ujao. Thamani ya udhamini wa NSM ni takribani 32,000,000/=.
"Mangement Forum ni fursa ya mameneja na wadu wengine wa mabo ya uchumi kukutana na kujadili mada inayotolewa na mzungumzaji ambae ni bingwa katika eneo fulani la uchumi au menejimenti.
"Hii ni mara ya nne katika siku za hivi karibuni kwa Ndovu Special Malt kufadhili shughuli za kuwaongezea umakini na maarifa wa kijasiriamali, kiuchumi na kifedha vikundi mbali mbali.
"Kwa vitendo hivi vinne vya udhamini Ndovu Special Malt inaendelea kuthibitisha kwamba kweli ni Chaguo Makini kwa ajili ya watu wanaojua ni nini wanachokitaka maishani na ambao wako makini kujiongezea mbinu maarifa ya jinsi gani ya kutawala mazingira yao ili kujiletea maendeleo.
"Udhamini wetu wa Management Forum una mwanzo mzuri kwa maana unaanza na kwa kishindo na magwiji wawili wa kimataifa wa maswala ya uongozi na mageuzi katika menejimenti- Philip Goodwin and Tony Page- ambao watazungumzia: jinsi viongozi wanavyoandaa viongozi, jinsi anvyotawala mabadiliko na jinsi wanavyoweza kufanikiwa katika haya katika mazingira yanayobadilika kila wakati.
"Uhusiano wa NSM na wasomi, wanataaluma, viongozi wa makampuni wa ngazi mbali mbali na wajasiriamali ni wa kudumu na tutaendelea kuwatangazia taarifa za mwendelezo wa ushirikiano katika shughuli zingine na vikundi na mitandao mbali mbali kati yao na NSM; kwa maana NSM ni chaguo makini, hivyo NSM ni yao".


MHE, MICHUZI,
ReplyDeleteNIWASILISHIE HUU UJUMBE KWA KAKA MPELI. JE KAKA YAKE CHARLES NSEKELA HAJAMBO? MIE NI RAFIKI WA ZAMANI NIKO MAREKANI KWASASA NA TULIPOTEZA MAWASILIANO. SHUKRAN.
FATMA MAHAMOUD.