juu mwenyekiti wa nccr-mageuzi mh. james mbatia anaoneshna kukata tamaa na kutojua la kufanya wakati mama martha ndunye akiangua kilio kutokana na hali ya mwanae kelvin katalama ambaye kalazwa katika taasisi ya moyo ambayo leo ndiyo siku ya mwisho wa notisi ya taasisi hiyo kuhama waliyopewa na wenye nyumba nssf kutokana na kutolipia pango. chini ni sehemu ya mapokezi ya taasisi hiyo. kwa mujibu wa mahojiano na tbc jana uongozi wa nssf umesema umeshafanya kila liwezekanalo kumaliza na mwendeshaji wa taasisi hiyo pekee binafsi ya moyo lakini ufumbuzi wa kulipwa hilo pango haujapatikana hata pale swala lilipofika kwa waziri husika. akiongea na waandishi muda mfupi kabla ya kutembelea wagonjwa waliolazwa hapo, mh. mbatia alimuomba jk aingilie kati sakata hili kwa kudai kwamba taasisi hiyo ni nyeti kiasi na haifai iachwe inataabika kwa jinsi inavyosaidia wenye kipato cha chini kupata matibabu ya moyo wakiwa nchini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 18 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 24, 2008

    Hapa kuna issue mbili. 1. kama taasisi hii ni Not for Profit, je kwa nini serikali isiisaidie majengo ili kuwapatia huduma watu wa chini?. Kuna uwezekano serikali inamtaka Dr. Masau afanye kazi muhimbili na yeye hataki. Ila kingine ni kwamba Jamaa aombe msaada kwa wafadhili atakuwa na credibility kubwa kuliko NGOs nyingine za kiulaji ambazo zinapewa mabilioni na wafadhili kama EOTF, WAMA na nyingine nyingi hasa zile za Briefcase.

    Ila Mbatia anapataka JK aingilie wakaki ana wakilishwa na Wizara ya Afya ambayo imeishindwa kuipatia THI ufumbuzi kwa sababu wanazozijua wao hii ni hatari kwa vipaji vilivyo nje ya nchi. Tanzania ina wataalam bingwa wengi wapo nje ya nchi ambao wanahofia kurudi Nyumbani kuendeleza nchi kwa kuhofia kutoungwa mkono na watu wasio wazalendo wanaoshikilia maamuzi ya hatma za professional Zao. Dr. Masau akaifungulie Botswana ili watanzania waanze kwenda Botswana kutibiwa moyo badala ya India

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 24, 2008

    Kapuya alipopata ajali tuliona picha yake akiwa Hospitali uso wote umevimba leo hii wagonjwa wa moyo wako hospitali anashabikia wahame ,imekaaje hii waugwana?
    Kama ni ndugu wa wakubwa wakiwa na matatizo ya moyo utasikia wamepelekwa India kwa fedha ya serikali.
    Watanzania safari bado ndefu na sijui kama tutafika.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 24, 2008

    this is ridiculous. Yaani taasisi nyeti kama hii serikali haiwezi ingilia kati na ku'bail out the institution? Private initiatives kama hizi zinabidi ziendelee kuwepo, na bila msaada wa serikali hatutaweza kusonga mbele. jamaa ameendesha kituo hicho kwa grant money za wafadhili wa nje tokea miaka hiyo. kwanini uongozi wa wizara ya Afya usiingilie kati na kupigania? tatizo ni kwamba nchi yetu, hamna mtu anayeweza pigania maslahi ya m(wa)tu mwengine, unless kuwe na ulaji. tunahitaji kusonga mbele. tuwe wazalendo na kufikiria 20-50 years ahead, leo hii mnamuachisha jamaa hatua aliyopiga ili wengine wafuate. sasa itabidi aanze moja kutafuta mahala pengine kwa kuendelea na kazi hiyo, itamgharimu pesa zaidi na muda. hivi nchi yetu inaongozwa na ma mbumbumbu? ama?

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 24, 2008

    Kwakweli hili jambo serekali inabidi waliingilie kati, ndani ya jengo kuna wagonjwa watawapeleka wapi jamani?

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 24, 2008

    Pole sana Dr. Masau, my common sense muda mrefu sana uliopita iliniambia you cant work in Tanzania,hasa ulipoanzwa kufwatwafutwa na watu Muhimbili na hasa maprofessa wenzako. Lakini kitu sensitive ni hili deal la kupeleka wagonjwa moyo India, huu ni mradi mkubwa sana wa Wizara ya afya,Ma-director na watendaji wengi wa wizara wametajirika na mchezo huu mchafu.Kingine ni kwamba ulikuwa unashindana na wahindi wa Lions Club.Kuna pesa nyingi sana wanapata kama fund!!!

    ReplyDelete
  6. AnonymousJuly 24, 2008

    HAPA LAZIMA KIKWETE AINGILIE KATI TENA TENA SI KWA UPANDE WA DENI TU BALIA HATA UJENZI. MJENGEENI HUYO MTAALAM HIYO HOSPITALI KAMA ANAVYOTAKA NA HILO DENI ASAMEHEWE ROHO NYINGI HAPO ZIMEPONYESHWA. HIYO NI TAASISI MUHIMU YAANI KWELI HUYO KAPUYA NDIO AKILI YAKE YA PUYA KAMA JINA LAKE dAA HII KWELI NGUMU.

    ReplyDelete
  7. AnonymousJuly 24, 2008

    Kuhusu suala la kuamisha wagonjwa ni vyema NSSF wangetumia ubinaadam,wasiwahamishe maana kuna hao wagonjwa wanaosubiri operation wangewaacha wafanyiwe kwanza sababu kama watawapeleka Muhimbili watapewa tarehe mpaka 2010 kutokana na hari ya pale na foleni zilizopo,na ujilikae kwa operation ya moyo mpaka inapokaribia kufanyika uchakato mrefu umefanyika ambao itabidi uanze upya uendako,shwala la pili huyu DR.MASAU anatakiwa abebelawama kwa hari yote ikiwamo kuwapa taharuki wagonjwa
    1.KWA NINI ATUMIE JENGO LA WATU BILA KULIPIA.
    2.ALIKUWA ATOI HUDUMA BURE JE,PESA YA KODI KWA NINI AKUITENGA.
    3.ANADAI AKULIZIKA NA NSSF WALIVYO FANYA UKARABATI WA JENGO JE KWA NINI ALISAINI MKATABA? YEYE AKIWA MSOMI NA MTAALUMA ALIINGIAJE KTK JENGO KUFANYA UTABIBU ILHARI ALIPO KTK VIGEZO STAHIKI?

    ReplyDelete
  8. AnonymousJuly 24, 2008

    Ikumbukwe kuwa Prof huyu alipatiwa kazi India walimtaka na kumuahidi mshahara mnono lakini alikataa kwa kusema kuwa anataka kuwasaidia watanzania, Kama NSSF ambao wanawekwa na michango ya wavuja jasho wanajali pesa kuliko maisha ya watu huu ni uwehu tuu, wangefikiria cha kumsaidia kwa wingi wa majengo ambayo NSSF inayo wanaweza kabisa kumpa kajengo kamoja kwani leo hii NSSF wakimnunulia nyumba Tabata wakampa wakasema ni mchango wao kwa jamii, nyumba ambayo ni 20m watapungukiwa na nini wakati hiyo 20m ni gharama ya kumfanyia uchunguzi waziri akipelekwa nje?
    Kuweni wastaara bana.

    ReplyDelete
  9. AnonymousJuly 24, 2008

    Inawezekana tunapatiwa habari za upande mmoja. Kama issue ni kodi ya pango tuelezwe pia kwanini wao hawataki kulipa? Mbona hospitali nyingine za binafsi zinalipa kodi kama kawaida? Au hiyo taasisi inatibu bure wagonjwa wake na kama ni bure nini cha bure sasa huko tanzania? Hivi walipewa notice ya kisheria kuondoka? KAma walipewa kwanini hawakujiandaa kuondoka? AU pia wanadharau sheria?

    Hofu yangu tusijekuwa tunailalamikia serikali na NSSF bila kujua ukweli wa mambo. TUambiwe ukweli wa upande wa pili kwanini hawatki kulipa hiyo kodi.

    ReplyDelete
  10. AnonymousJuly 24, 2008

    sometimes nasisi tuache unafiki, hii dunia lazima siku moja tukubali kuchukua hatua zakisasa. huwezi kuendesha taasisi kisanii, nakama huwezi bora uchukuwe mkopo or ujuwe unataka kufanya nini, badala yake ndio hayo sasa.

    Mwishowe inaonekana NSSF na wizara ambayo ndio wakosaji wakati wazi kwao wao wanadai mapesa yao. this is business, kila mtu anataka faida. Jamaa naye anakula pesa kifisadi kwani hao wagonjwa wanalipia kwanini asilipie kodi ya jengo bwanaaa??

    Upande mwengine naomba serikali kupitia wizara husika iwape muda wakutosha hao jamaa wamalizie kuwashughulikia wagonjwa then wajuwa what next, hatuwezi wote kuwa wabaya.

    G7
    UK

    ReplyDelete
  11. AnonymousJuly 25, 2008

    mi nishatibiwa hapo bure sikuwa na uwezo wa kulipia na hali yangu ilikuwa mbaya sana,hivyo walishikwa na huruma na kunitibu bure,hapo wagonjwa wengi wanaopelekwa ni wale wasiojiweza kiuchumi hivo naona ndiyo sababu ya yeye kushindwa kulipa kodi.
    pia ule mradi wa kupeleka wagonjwa india kuna vigogo wengi wametajirika kupitia kukusanya ela kwa wafadhil ivo kuja kwake uyo kufanya upasuaj tanzania kaaribu ulaj wa watu.
    umuhimu wake tunauona si wa hali ya chin wenye nazo wanaenda kutibiwa nje.tanzania inasikitisha sana sasa uyo waziri wa afya ni kwa ajil ya wananch au wenyench ambao ni wala nch?
    tanzania inaitaj kuombewa dua kila siku il viongoz wabadilike.
    vijisent vingetosha kumjengea jengo kubwa kwa manufaa ya watanzania wote ila neno ufisad ndilo linatawala kila siku.
    tanzania bado,na uhakika anaofanya upasuaj akienda nch yeyote ulimwengun lazima atapokewa kwa shangwe na awez kosa ajira yenye mshahara mnono,ila kajitolea kuwa mzalendo ndiyo ivo tena!!!
    ndiyo maana walioko nje awaj kuwekeza tz sababu ya chuk binafsi na roho ya kwa nin na watu wachache kujilimbikizia chapaa

    ReplyDelete
  12. AnonymousJuly 25, 2008

    DR,MASAU DAWA YA DENI NI KULIPA SIO KULALAMA.

    ReplyDelete
  13. AnonymousJuly 25, 2008

    KAMA TUNACHANGIA WATU KWENDA ".INDIA." KWA MATIBABU..KWANINI HICHO KITENGO KISICHANGIWE ??? ACHENI ".UFISADI." MMEONA HAMTAPATA FEDHA KWA MGOGONGO WA KUWAPELEKA WAGONJWA ".INDIA." SIKU ZIJAZO KWASABABU WANAINCHI TUMEAMUA ".KUSOMA." NA ".KUJIZATITI." KUWA NA VITENGO VYETU HAPA TANZANIA (NYUMBANI).

    ReplyDelete
  14. AnonymousJuly 25, 2008

    Namuunga mkono G7. Kwanini tunapewa taarifa ya upande mmoja tu?. Tumeambiwa Dr Masau amekataa kulipa kodi kutokana na ukarabati kuwa duni,je kwanini alisaini mkataba wakati ukarabati ni duni?. Pia tumeambiwa anondolewa kutokana na amri ya mahakama. Kwanini asikate rufaa mahakama ya juu?. Au hana wanasheria wa kumshauri?. Isiwe ndio ameboronga na sasa anataka HURUMA ya Watanzania.

    ReplyDelete
  15. AnonymousJuly 25, 2008

    anyeumia ni mgonjwa mi naonea huruma sana wagonjwa pls serikali yote itupie macho swala hilo

    sweet,

    Arusha.

    ReplyDelete
  16. AnonymousJuly 25, 2008

    Mimi kitu kinachonishangaza kupita vyote ni jinsi watanzania wanavyopenda kukimbilia serikali kila kukiwa na tatizo...alafu mwisho mnalalamika kwa nini serikali inakuwa na nguvu hivyo na mafisadi wengi! Hapa nampinga huyu Mbatia kabisa. Hili ni swala la mahakamani. Kuna remedies nyingi mahakama itakayoweza kutoa kwa hii kampuni. Inaweza kuishikilia hii NSSF isiwatoe kwa muda, nk. Sasa kama mahakama haiwezi basi rule of law tanzania ni iko nyuma sana. Mimi sidhani kama hili swala ni la serikali. Hapa kuna contract na breach of that contract. Lazima mtu alipe. Lakini huyu mdau July 25, 2008 6:47 AM amesema safi...kama kesi imedunda mahakamani na haki imetendeka kweli, basi hakuna lingine. Kazi ya serikali na mahakama hasa ni nini?Nakubaliana na nyie mtakaosema serikali itete wanyonge, lakini pia kuwe na limit hapo...au sio? Lazima uruhusu biashara zitendeke bila kuingiliwa na serikali...au bado tuko kwenye ujamaa?
    Kusema kweli hii hospitali ina benefit kubwa sana kwa jamii...sasa sijui judge kaangalia kipi na kuona kipi. Hizi kesi zinahitaji kutolewa wazi kwa watu kusudi wananchi waweze kujadili na kuona kama kweli hawa ma-judge wanafanya kazi au la! Maana mahakama nazo zimekuwa taasisi za rushwa!

    anon of anon

    ReplyDelete
  17. AnonymousJuly 25, 2008

    NSSF wanataka kutuambia nini?Kwamba wao hawatambui unyeti wa huduma za Tiba ya Moyo?Kuna hospitali ngapi hapa nchini zinazo toa huduma ya Upasuaji wa Moyo?Hivi kweli nchi tuna viongozi wenye akili kweli?Utawezaje kulifumbia macho suala tete kama hili na huku ikieleweka kwamba Watanzania wengi sana wako kwenye 'waiting list'ya kupatiwa Tiba hizo za maradhi ya moyo,na pesa nyingi sana zimekuwa zikitumika kuwapeleka wagonjwa hao nchini India na kwengineko?Kama tungekuwa na viongozi wanaotumia akili TAASISI YA MOYO YA DR.MASAU ingekuwa inapewa Ruzuku na Serikali kila mwaka kwa kuthamini mchango wake kwa Taifa hadi hapo Serikali yenyewe itakapo jenga Hospitali yake yenyewe kwa ajili ya Tiba za Moyo.Ipende isipende kila mwaka Serikali inawajibika kuhakikisha kwamba Watanzania wote wenye maradhi ya Moyo wanapatiwa Tiba hiyo iwe hapa hapa nyumbani au katika Hospitali za Nje.Sasa kama hapa nyumbani Serikali bado haijakamilisha Taasisi kama hiyo ya Tiba ya Moyo IWEJE LEO SERIKALI HIYOHIYO ISUBUTU KUCHEZEA SHILINGI CHOONI?Who could be behind this Sabotage?Is the President of this Republic totally BLIND about this nasty episode which could backlash into his own premises?Je,Rais wetu anasubiri mpaka apelekewe Taarifa kuhusu Sakata hili?Yeye mwenyewe halioni na hajalisikia bado?MAMBO YA AIBU KABISA.Huu umaskini mpaka wa akili utatupeleka pabaya.Mimi binafsi nampongeza sana tena kwa dhati kabisa Dr.Masau kwa Roho ya Jabali kwa kutokubali kukatishwa Tamaa na Wapumbavu wachache?Tupo macho tunasubiri tuone Busara za Viongozi wetu.NA SITASHANGAA!

    ReplyDelete
  18. AnonymousJuly 25, 2008

    Its a shame. I mean its a BIG shame to see what we are going through. THI wake up?! Dont you see how serious this issue is? Dr. Masau we know something can be done. Please continue to save the lives of those people sicking in there. The fear itself will kill the most. Where is Kikwette in this issue.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...