deo mwanambilimbi na bendi yake ya kalunde ambayo inakuja juu kwa kasi kubwa
deo akiwa na mkongwa kyanga songa ambaye kajiunga nao hivi karibuni
pamoja na kuimba kwa umahiri kyanga songa pia hupiga gitaa kwa ustadi mkubwa
papaa akila mpini
jamwaka anaungurumisha bezi
ngoma na kinanda vipo mikononi mwa wakongwe hawa
safu ya ushambuliaji imesheheni kinadada wakali kwa kuimba. hawa ukiwataka kwa shughuli yako wala usipate taabu. piga simu ya mkononi +255 755 505 980 utawapata


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 11 mpaka sasa

  1. Kaza buti bwana Deo maendeleo yako babu kubwa na ndio tunavyotaka miziki ya Kibongo ipate chati kwanini kila siku sie wa mwisho? Hee jamani hata muziki lakini ipo siki tutatoka tuuu

    ReplyDelete
  2. Happy to c The Legend Kyanga Songa,We miss ur voice big time,since Tancut Almasi.
    KEEP IT UP DEO,KAZI NZURI INAPENDEZA.
    Cha chandu- UK

    ReplyDelete
  3. Nimefurahi kumuona KYANGA SONGA, NI SIKU NYINGI TOKA IRINGA NA TANCUT ALMASI, HAWA WALIKUWA MAPACHA, MMOJA ALIMUOA DADA MMOJA WA BENKI NBC AKIITWA JANE BUTININI NI MHAYA WALIOLOWEYA IRINGA, MARA YA MWISHO ALIACHISHWA KAZI NBC NA ALIJIUNGA NA JESHI KWA VILE ALIKUWA MKALI WA NETBALL, MMEWE ALIKUWA ANAITWA KASALOO KYANGA SONGA, NI KATI YA HAO MAPACHA NDIYE ALIYEKUWA NA SAUTI NZURI MTU WA KUJIPENDA HIVI KWA SANA, SASA SIJUWI NI HUYU?

    ReplyDelete
  4. jamani hee!! ina maana huyu Kianga Songa ni wale mapacha? he amezeeka kweli hivi wadau mnaweza kunijulisha pacha wake yu wapi? nakumbuka enzi zao walivyokua wanatesa pale jasmina kijitonyama, kweli ya kale dhahabu, na huyu deo yeye ni nani? ila Michuzi hebu tutafutie picha za kina KIkumbi Mwanza Mpango Mema Yani mzee mzima KING KIKI, enzi zake na masantula ngoma ya mpwita, na akina Frida, Ngalula, jamani kweli walitesa sana, japo namzimia sana mzee KIKI hadi sasa, jina kubwa hilo ukizungumzia sanaa ya muziki wa TZ, ni sawa na wakongo wanavyomuheshimu PAPA WEMBA, eeh kwa kweli mambo yalikua muswano sana enzi hizo.

    ReplyDelete
  5. Mkimtumia vizuri huyo Kyanga na kumpa heshima yake kimaslahi Deo mtafunika muda si mrefu.Huyo Kyanga ni Balaa kwa Muziki.Walipokuwa na nduguye Kasaloo ulikuwa ni mshikemshike Fimbo Lugoda!

    ReplyDelete
  6. hivi kianga yule nduguyo kasoloo kianga yuko hai?

    ReplyDelete
  7. Hivi wewe chachandu up wapi ndani ya UK?
    yaani kila nikiona jina lako napatwa nakiwewe cha kukuona chachandu.
    sema basi tukujue then....

    G7
    !!!!!!!!

    ReplyDelete
  8. Wadau naomba kuuliza kwani KASALOO KYANGA bado tunae hapa DUNIANI? Naomba jibu sahihi kwa wanaojua

    ReplyDelete
  9. Michuzi pole na kazi mkuu...Naomba nikusahihishe kidogo..Huyo bwana ni KASALOO KYANGA na si KYANGA SONGA..KYANGA SONGA kwa sasa ni marehemu ukitaka taarifa zaidi mfuate KASALOO umuulize maana yhe KALUNDE BAND kila ijumaa na jumatano wanatumbuiza PEACOCK HOTEL Mnazi Mmoja na kila Ijumaa na Jumapili wanapiga GIRAFFE OCEANIC VIEW Mbezi Beach ambako ni karibu na wilayani kwako Tegeta

    ReplyDelete
  10. bro michuzi kama kuna wakati umechemka basi ni huu.kwanza nenda ukamwombe radhi huyo bwana aliyeshika gitar kwa sababu yeye siyo kyanga songa bali yeye ni kasalo kyanga.kyanga songa alikwisha fariki muda mrefu!.usiwachanganye wasiomfahamu!

    ReplyDelete
  11. Waama! Huyo ni Kasaloo Kyanga, pacha wake Kyanga Songa alifariki tangu mwaka 2000.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...