Makamu wa Rais Dk. Ali Mohamed Shein katikati akila futari pamoja na Wananchi wa Kisiwa cha Pemba aliyoiandaa kwa ajili ya Wananchi wa Kisiwa hicho huko katika Ikulu ya Chakechake jana. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Mh. Juma Kassim Tindwa kulia Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Mh. Dadi Faki Dadi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 13 mpaka sasa

  1. Salaam Aleikhum wadau mimi nauliza Rais na Makamu wake wanapofutarisha watu hizi pesa huwa ni zao mfukoni au za Serikali hapo sielewi nisaidieni jamani maana mimi mwenyewe huwa najaribu kwa Familia na joto ya jiwe naliona je hawa wakubwa vipi?

    ReplyDelete
  2. Sheikh Issa nbona lugha unaiharibu?

    Futari= chakula cha kufungua swaumu

    Futuru= kitendo cha kufungua swaumu

    FUTURISHA = ni kitendo cha kuwafungulisha swaumu waliofunga na sio KUFUTARISHA

    ReplyDelete
  3. Ni kwa nini futari hailiwi mezani?Ndiyo,zamani jamii zetu zilikuwa hazina mambo ya meza na viti,pia msikitini HATUSWALII kwenye viti kama wakristo TUFANYAVYO.Sasa ni kwa nini futari nayo iliwe kwenye majavyi while we aint in the msikiti?Naomba mnisaidie

    ReplyDelete
  4. salaam,ndugu mbigiri hiyo tabia ya kula chini ni sunna kwa waisilamu na sio kama unavyofikiria labda ni umaskini au vipi nadhani utakuwa umenielewa.

    ReplyDelete
  5. raisi anapofuturisha wananchi, hutumia fedha zake mwenyewe, au fedha za serikali?

    ReplyDelete
  6. Mbona hamuulizi mapambo ya krismas kwenye majengo ya serikali yanatoka wapi?Mnauliza futari tuu!!

    ReplyDelete
  7. Futari na futuru inategemea ulipo.

    Unguja tunasema saa ya kufutari
    Bara wanasema saa ya kufuturu

    Lengo ni hilo hilo moja

    Sisi tuna tungule
    bara mna nyanya.

    Ukija Unguja baada ya muda utazoea, na muunguja akienda bara baada ya muda keshazoea, kwahio Michuzi alivyoandika hakuna kosa lolote

    ReplyDelete
  8. najuwa sio umaskini,Nachouliza ni kwa nini suna haiwezi kuliwa mezani?

    ReplyDelete
  9. Fungu la futari hiyo linatoka ofisi ya makamo wa raisi

    Unguja kuna mfereji
    Bara kuna bomba
    Unguja kuna msingi
    Bara kuna mtaro
    Mmenifahamu hapo??

    ReplyDelete
  10. Mbigiri jifunze kwanza maana ya suna


    suna = nikitu kilichopendekezwa lakini ukikosa haidhuru kupata thawabu,
    suna= ukifanya hivyo ndio unaongezewa kidogo katika thawabu zako.
    Kwahio futari inaweza kuliwa mezani na ukapata thawabu.

    ReplyDelete
  11. Suna siyo chakula wewe, suna ni mwenendo wa Mtume. Kwa hiyo wanafanya hivyo kwa sababu Mtume alifanya, lakini najuwa unafahamu wanaweza kuwa na fenicha kali zaidi ya zako, si umeona vyeo?

    Wengine wasiojisikia kufuata suna hupasha mezani si neno.

    Na ukiweka mabenchi utarukuu na kusujudu vipi?

    ReplyDelete
  12. ndugu mbigiri bado nipo na wewe bega kwa bega,sunna ni jambo ambalo ukifanya unapata thawabu ukiwacha kufanya hupati thawabu wala dhambi you get me,kama vile kula kwa kutumia mkono, mtume wetu muhammad (saw) ametuhimiza wakati wa kula tutumie mkono kuliko kijiko, sababu moja kubwa unapotumia mkono unakifanya chakula kiharibike upesi kabla ya kufika tumboni.mpaka hapo utakuwa umenifahamu tosha japo kuwa umeuliza wewe lakini faida wamepata wengi,ramadhan kareem.

    ReplyDelete
  13. Kama ukisema kiharibike upesi watu wanaweza wasielewe, basi Digestion. waende kusoma kamusi. Digestion inaanzia mkononi.

    Experiment: pika cahkula tufanye maharage, kisha pakuwa kwenye bakuli mbili. Moja gusa maharage kwa vidole nyengine usiguse. Yaweke baada ya muda, maharage yaliyoguswa yataanza kutoa harufu ya kuchacha.

    Kuna bacteria mkononi? ndio lakini hawana madhara ni kama wale wa chanjo. Wengine wamejaa mwilini lakini sio wa maradhi.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...