Ras Makunja akiwajibika

Nicheke ninenepe!

wakati mjadala unaendelea kuhusu vekesheni ya balozi wa nanihino ambaye pia ni mkuu wa wilaya ya Nanihii, Kaka braza kakimbilia studio kufyatua wimbo mpya uliobeba jina la "Kizabi Zabina" si mtu Mwema!

Kizabi zabina huyo alitajwa kwa jina la Binti Pazi au Mzee pazi, analalamikiwa na kiongozi wa bendi ya ngoma africa ras makunja kwa kuigombanisha jamii na kuwa sumu ndani jamii.

Wadaku walioshuhudia madongo makali yalikuwa yakirushwa na mwanamziki huyo katika studio huko ughaibuni.wamebaki midomo wazi kutokana na uzito wa madongo na hoja zilizojaa ukweli ukweli kuhusu "Kizabi Zabina", huyo Bint Pazi aka Mzee Pazi.

Kiongozi wa Ngoma Africa Ras Makunja kamshitaki kwa jamii "Kizabi Zabina" kwa kosa la kuichonganisha jamii, tena kampa Shua kwa kumwambia "atafute la kufanya" na "kuwekeza mda mwingi katika maendeleo".

Watafiti wa mambo wanadai kuwa Ras makuja na kitu kipya hiko "Kizabi Zabina" kinaifanya bendi ya The Ngoma Africa yenye maskani ughaibuni kuonekana kuwa karibu sana na jamii ya Uswahilini kwa tungo zake ambazo mara nyingi zina elimisha,au kuishauri jamii ,wakati mwingine ni mwaliko wa malumbano ya hoja .
-MDAU MSEMAKWELI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 14 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 27, 2009

    KIZABI ZABINA NI BENEDICT MWAKYANJALA MAARUFU KAMA MWANAKIJIJI AU KADA WA CHADEMA TAWI LA JAMII FORUMS.
    MDAU MSWAHILI.

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 27, 2009

    Yusuph mzee wa jahazi modern Taarab aliimba wimbo unaitwa two in one au MPEKEPEKE.
    hivyo tumbatize Mwanakijiji kuwa ni MPEKEPEKE. na jamii forums yake.

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 27, 2009

    haya jamaa sasa huyu ras makunja,anatuacha hoi na hii mpya yake! lakini sidhani kama anamlenga
    Mwakyanjala.Lakini makunja hizi ndizo
    zake akawizi mambo.
    Kinachonishangaz ni wimbo huu wa kizabi zabina,mbona yeye mwenyewe watu hawamlalamiki kwa tabia zake za kuwarushia watu madongo.

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 27, 2009

    mdomo wa kaka bro ras makunja kweli haukawizi mzozo,ukisikia uwanamziki ndio huu!? ndogo juu ya madongo.Kaka rusha madongo

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 27, 2009

    hiiiiii!!!!!!te te! kamanda Ras makunja,nakukubali kazi zako ni muhimu kwa jamii hii ya wabongo,siku hizi fitina,majungu yapo mpaka kwa watu tunaowaita WASOMI,badala kuleta maendeleo wao ndio wapo mstari wa mbele katika fitina na majungu,bora ulivyohamua kuwafungia kibwebwe

    ReplyDelete
  6. AnonymousMay 27, 2009

    hapa braza kaka ras makunja !!!!!!unanipa kigugumizi na kazi yako ya Undewa au mjumbe wa kuhamua maswala ya jamii!!!! hule ugomvi wa wafanyibiashara juzi tu ulichomoa kibao kipya FURAHA YA MAISHA IKO WAPI? sasa hili soo la vakasheni ya misupu naona unarusha dongo jingine! ninakupigia saluti.

    ReplyDelete
  7. AnonymousMay 27, 2009

    mmmmmmmmmm!!!vakasheni ya balozi kweli imezua mambo.sasa kesi hipo kwa jamii? mungu wangu,nangoja nimsikilize ras na ffu wake wanapompiga virungu kizabi zabina.
    kweli ngoma inogoge

    ReplyDelete
  8. AnonymousMay 27, 2009

    hiiiiiiiiii leo ! Kizabi zabina mzee Pazi kakumbana na ffu..........sasa kazi hipo,ras rusha mawe yamfikie huyo kizabi zabina

    ReplyDelete
  9. AnonymousMay 27, 2009

    Ras Makunja kwa nini? kesi hii msipeleka mahakamani badala yake mnaanza zogo kwa kuwapa waswahili wahamue?wakati wewe mwenyewe unajua wazi huku uswahili Vizabi zabina ndio kwao.Kaka naona umedhamiria kuleta zogo uswahilini.
    lakini we haya tutafika tu

    ReplyDelete
  10. AnonymousMay 27, 2009

    hii imekaaje? tulisikia nyie ngoma afrika siku hizi mna adabu na hakuna tena kurusha mawe?sasa huyu mzee pazi mbona anatupiwa matofali?jamani msalieni mungu

    ReplyDelete
  11. AnonymousMay 27, 2009

    hii bwana nzee kizabi zabina na bw.kichwa ngumu hili ni soooo la kukata na mundu,sasa tuone nani ?mwenye haki.ngoma afrika mna mdomo!haki ya mama

    ReplyDelete
  12. AnonymousMay 27, 2009

    hili bifu la nguvu ffu na mzee pazi,mie yangu masikio.
    Mdau wa msondo,Buguruni.

    ReplyDelete
  13. AnonymousMay 27, 2009

    kizabizabina si mtu kabisa kwa nini? Michuzi unakaa meza moja na kizabizabina na kula naye msosi.
    sasa unaona maneno yamefika kwa afande na kamanda anayepeleka adharani.

    ReplyDelete
  14. AnonymousMay 28, 2009

    mzee kizabizabi na kaka mwenye gubu kubwa,ngoma uwanjani

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...