Muhula wa Pili wa WaPi Zanzibar umewadia....

WaPi ni tamasha la sanaa linalofanyika kila mwezi. Tukio hili linakusudia kutoa nafasi kwa wasanii wanaochipukia kushiriki na kuthibitisha vipaji vyao.

Katika Muhula huu tunakusudia kuanza kulipeleka tuko hili katika baadhi ya shule ili kuchochea ushiriki wa wanafunzi zaidi katika mijadala na sanaa. 
Tunatarajia pia kushirikiana na baadhi ya taasisi mbalimbali ili kutoa nafasi za kujiendeleza kitaaluma na kisanii kwa wale watakaoonyesha juhudi na mwelekeo mzuri.

Tukio jingine jipya katika muhula huu ambalo litawezeshwa kama kawaida na BRITISH COUNCIL ni ubunifu na usanifu mitindo.

Mada ya safari hii katika WaPi ni USHIRIKINA...maafa kwa Maalbino... Tunatarajia kushirikisha wadau mbalimbali katika kujadili namna Ushirikina ulivyochangia katika ongezeko la maovu na pia kuangalia kama una manufaa au la.

PROGRAMU ITASHIRIKISHA:

Waongozaji wa tukio kutoka WaPi Zanzibar

 DJ Cool Para

Jukwaa la sanaa za Mikono

Matona kutoka DCMA atatoa ufafanuzi wa awali juu ya nadharia ya muziki wa Mwambao kwenye Kona ya MAARIFA 

JAMBO CABARET katika uchezaji na sarakasi

Mjadala wa mada

USHINDANI WA MAEMSII

Mtaalamu wa kupiga Qanun Nasor atakuwepo pia

Ngoma asilia

Shindano la vichekesho

PAMOJA NA SIZA MAZONGELA WA SEGERE 

Mengineyo ni pamoja na Tenzi, Upambaji, Uchezaji na upigaji wa ala mbalimbali...

MAHALI NI NGOME KONGWE

Jumapili tarehe 03-05-2009 kuanzia saa 9 alasiri hadi 2 usiku

Hamna kiingilio

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 02, 2009

    Zafara...you guys are doing such a good work...well done all the people involved. It's been long time coming...

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...