Tamasha la fasihi na
maadhimisho ya mwaka mmoja wa Soma.

Soma Mkahawa wa Vitabu unawakaribisha kujumuika nasi katika tamasha la tatu la fasihi litakalofanyika sambamba na maadhimisho ya mwaka mmoja wa Soma kuanzia leo Ijumaa, Jumamosi hadi Jumapili.
Shughuli na maonyesho mbalimbali yatafanyika ikiwa pamoja na maonyesho ya kazi mbalimbali za usomaji na uandishi wa fasihi, kazi za ubunifu, mijadala ya kirika na masuala ya kijamii, simulizi za hadithi, tambo za kishairi, maonyesho ya vipaji kwa watoto na vijana, filamu fupifupi.
Kutakuwa pia maonyesho lukuki kutoka kwa wasanii na wanafasihi maarufu kama MRISHO MPOTO, VITALIS MAEMBE, ROGERS LUCAS na wengineo wengi watajumuika pamoja na kutumbuiza pamoja na wasanii wachanga katika siku zote hizo tatu za tamasha.

Unakaribishwa kuja na tungo, mashairi na kazi zinginezo za kifasihi na kisanii ambazo ungependa kuzionyesha na/ama kuzijadili pamoja na wadau wa jamii ya usomaji, ubunifu na utamaduni.

Jumamosi tarehe 11 Julai 2009, Saa 4 asubuhi hadi saa 12 jioni
Jumapili tarehe 12 Julai 2009, Saa 9 jioni hadi saa 2 usiku.

“Karibu Soma ujenge maarifa,
ufurahie utamaduni
na uburudike katika mandhari murua”

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 13, 2009

    ni kweli

    mana tulio wengi kiswahili hatujui kabisa,sasa ndo usiseme vijana wa kizazi kipya sasa ndo zero kabisaaa

    yan ilimradi mtu naunganisha tu sentensi na unaelewa basi

    kazi ipo adi tufike!!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...