Furaha kama hii ya simba kutwaa kombe itajirudia tena???

Mpambano wa watani wa jadi washington Dc,homa yazidi kupanda,huku Simba wakitamba kwamba watakirudia kile walichokifanya april 26 mwaka huu,kwa kuirarua Yanga 3-2,katika mechi iliyochezwa Meadowbrook park kusheherekea siku ya Muungano.
wakiwa kambini na mfazili wa Simba,Said Nasoro wachezaji na viongozi wa timu hiyo mtaa wa masimbazi,wamesema ushindi ni mkubwa sasa hyo jumapili tunawapiga goli 5-0,Yanga wanajaribu kubadilisha uwanja kwa kisingizio kwamba uwanja ulikua mbaya. yaani hata waende wapi...waisha elekea kibra.
mpambano huu,ambao umepangwa kuchezwa jumapili sept 6 kwenye uwanja uliopo kwenye kona ya 16th st,na kalmia st,umeleta vitimbi vingi,uongozi wa Yanga umedai ulimkuta uwanjani Bamchawi(Mkakile) akifanya vitu nyake,hii mechi watu wanataka kuuwana alidai uongozi huo,sis tunacheza mpira wa sayansi na teknologia. Simba kawaida yao kutangaza ushindi kabla ya mechi.
katika kambi ya Yanga mambo ni swari,na timu inaendelea vizuri na mazoezi chini ya kocha mpya Yasin Manyoka,Uongozi na wachezaji walikua kimya hawakutaka kuzungumzia mpambano huu wa kukata na kisu,unaosubiriwa na mashabiki DMV na vitongoji vyake,labor day weekend,msema ukweli ni dakika 90.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Hakuna jumuiya ya watz iliyo nje ya wazugaji kama hii ya DC,hawa jamaa ni wasanii kweli kweli na kila mmoja wao kwenye mind yake yeye ni kuhusu kutengeneza hela kupitia visikukuu kama hivi!

    Nina uhakika na hiki nisemacho,maana wao wakija kwenye majimbo ya wenzao huwa wanahudimiwa sana,lkn wao wakiita watu wa majimbo tofauti huwa wanawakimbia wageni!

    Huwa wanakwenda Houston kila mwaka kwenye thx giving na huko huwa wanakula na kusaza,na muziki bure,lkn Houston walipokuja kwao mambo waliyowafanyia ni aibu kusimulia!

    Kwa ufupi hawa jamaa waache usanii wa kutumia sherehe hizi kama ndiyo njia ya kuongezea kipato

    ReplyDelete
  2. MICHUZI KUNA JAMAA KULE ALIKUPAKA NIKAKUTETEA LKN BADO TU UNAENDELEA KUTUKERA KUHUSU HAWA JAMAA ZAKO UNAOTUWEKEA PICHA ZAO NA MGAZEETI MREEEEEEFU TUWASOME WAKATI HAWA MPIRA HAWAJUI NA WASHAZEEKA WEE HUONI HATA HAWAPATI COMMENTS.ACHANA NAO WACHUNIE WAUZA SURA TU HAO MPIRA HAWAJUI NAFUU UTUWEKEE PICHA ZA LIGI KUU YA BONGO KULIKO HAWA VILEMA

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...