Kwa jina anaitwa Chege Chigunda kutoka kundi la Tmk Family akikamua peke yake jukwaani bila ya baadhi ya wasanii wa kutoka kundi hilo na kufanya vyema kabisa kwa mashabiki wao ambao walionekana kumshangilia kwa kiasi kikubwa Chege
Msanii mahiri wa Hip Hop kutoka kundi la Familia,Chid Benz akionesha umahiri wake wa kufloo mitindo huru a.k.a Free style mbele ya mashabiki wa tamasha la fiesta ambalo lilifana sana mwishoni mwa wikend.
Msanii mkongwe wa muziki wa kizazi kipya Prof Jay akikamua mbele ya umati mkubwa wa wakazi wa mji wa dodoma waliofika kwenye tamasha la fiesta mwishoni mwa wiki
Umati wa watu ukiwa ndani ya tamasha la fiesta one love 2009,ambalo limefanyika mwishoni mwa wikend ndani ya uwanja wa mpira wa miguu wa Jamhuri mjini Dodoma.Tamasha hilo linaloandaliwa na kampuni ya Prime Time Promotions na Clouds Fm ndio limeanza kutimua mbia zake rasmi na wiki ijayo litafanyika mjini Arusha.Kwa picha zaidi kuhusiana na tamasha hilo bofya hapa

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 9 mpaka sasa

  1. safi sana vijana mimi nawafagilia pamba kwani kila siku mnakuja na ubunifi ila hizi za sasa zimetulia mnavaa kama mko USA

    ReplyDelete
  2. kweli tanzania ni nchi huru yaani watu wanajirusha watakavyo

    ReplyDelete
  3. tunaomba matamasha kama haya kila mkoa kwani yanatuunganisha watanzania ok

    ReplyDelete
  4. nani apewe credit kwa vazi la kitambaa? Alafat wa PLO, Kanumba au kuna mbunifu mwingine maana naona sasa kila Kona. Pia nashauri haya matamasha yawe yanatoa report ya mahuduhurio na pesa iliyokusanywa, kondom zilizouzwa, bia na sigalla ni muhimu sana kudocument vitu kama hivi

    ReplyDelete
  5. kweli show nzuri. Ila mie niko kinyume kidogo na hawa wanaoitwa kioo cha jamii. Hivi kwani kila kitu kuiga jamani?? Sifurahishi na tabia ya kuiga bila kujiuliza kwa kina dhumuni la alienzisha ama kuonekana na kitu fulani. nikiwa na maana kwamba. waliiga kujishikashika mbele ya nyeti zao wawapo jukwaani kama waanzilishi walivyofanya. sasa wameibuka na vitabaa shingoni eti ni mtindo, Jamani naomba kuelimishwa. binafsi nilichukulia kwa washika nyeti wa kimarekani wawapo jukwaani kuwa pengine kuna ka muwasho sehemu hizo, ama suruali zao ni ndefu kiasi cha kuwafanya wapandishe kila muda tena kwa upande wa hadhira. Swali je nikiwa sahihi, na wobongo flava nao wanawashwa sehemu nyeti? ama suruali zinashuka japo hata wavaa kaptula hufanya vivyo hivyo?
    Pili kwa kitatambaa shingo nilidhani kwa ajili ya baridi ama kujifuta jasho ,na hawa wana kwetu je? mdau scandnavia.

    ReplyDelete
  6. Anony Mon Sep 28, 03:03:00 PM kuna vingapi umeshaiga hadi leo?
    unaja hata kuvaa nguo sio asili ya mwafrika?
    nini ambacho hujaiga ktk maisha yako?
    Acha kupaka-ila shauri kwa busara na nia nzuri

    ReplyDelete
  7. Be honest ninyi hamuigi?
    Hujaiga kitu?
    Suliali, shati nk vyote umeiga
    So wat ar u toking abt?
    Acha vijana wajirusheeeeeeeeee

    ReplyDelete
  8. kussaga,Mohamed Dosidosi na Oscar Mziray wako Wapi?

    ReplyDelete
  9. MDAU WA SCANDNAVIA UMESEMA!!!!!...HAHAHAHAHA...AIGIZAYE TEMBO KU***A ......HAHAHAHAAAAAA

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...