Habari za kusikitisha zilizopatikana mapema leo,zinaeleza kuwa mvua kubwa ilionyesha wilayani Same mkoani Kilimanjaro usiku wa kuamkia leo,imesababisha maporomoko ya ardhi na kupelekea maafa ya watu wanaokadiriwa kufika 25 ,taarifa zinaeleza kuwa maporomoko hayo yalizikumba nyumba saba zilizokuwa na watu,ambao walikuwa usingizini,katika kijiji cha Goha,wilayani Same.
Hadi jioni hii inaelezwa kuwa jumla ya maiti 15 zimeshapatikana na miongoni mwao 10 ni za kike na 5 ni wa kiume. Jitihada za kunasua maiti nyingine bado zinaendelea.Kwa habari zaidi baadaye kidogo.
uwi kiru yesu wangu weee,Tina wa new york tumefiwa sisi huku home na mama,pamoja na baba katika mafuriko haya,yesu wangu tina pokea simu yako please..mimi Anita..
ReplyDeleteooh my God, this s terrible...
ReplyDeletepolen sana mliofikwa na maafa na wengine wa mabondeni na sehemu nyingne hatarishi kuepukana na matatzo
Kama warning zimetolewa sn kuhusiana na mvua zinazotarajiwa (elnino).
Mungu awa rehemu wote.
Jamani sasa watu waende wapi??? Sehemu kama Kinodoni maji yanajaa vile vile hata sehemu nyingine sio mabondeni.
ReplyDeleteNi kuwa viongozi wa serikali za mitaa waboreshe miundombinu. Wasimamie ipasavyo.
Mfano tangu mvua hizi zianze kutangaziwa sijaona badiliko lolote ambalo serikali hasa hawa viongozi wa mitaa wakifanya.
Mitaro bado imejaa vile vile, hakuna lolote lililofanywa kuhusu usafi na uzibuaji.
Hakuna mafunzo yoyote yaliyotolewa kuhusiana na majanga ya mafuriko kama ilivyo nchi nyingine wanavyofanya.
Mfano mzuri Malawi ni nchi pia moja bado changa lakini wanatushinda sie, wao weshaanza kuwafundisha wananchi jinsi ya kukabiliana na majanga ya mvua.
Naamini hapo ni kuilaumu serikali hakuna wakulaumiwa zaidi ya wao.
Wao ndio wangetakiwa kutilia mkazo ikiwezekana viongozi wa mitaa wapite wahakikishe kila mitaa yao watu walio katika maeneo hayo wapo katika hali iliyo salama ikiwamo kucheki je nyumba wanazo ishi ni salama kukabiliana na mvua kubwa kama sivyo wawape notice wahame na je kila mtaa mifereji iliyopo inakidhi kupitisha maji mengi? Kama haikidhi wajikusanye hata kushirikiana na wananchi wasafishe mitaro na kuipanua zaidi.
Hakika hawa viongozi wa serikali yetu ya Tanzania wamekuwa wakilala sana. Wananikinaishaaaaa.
Poleni sana jamani.
ReplyDeletejana tu nilikua naangalia news nikaona haya maporomoko yametokea huko TN. Nikajiuliza hivi mbona Tanzania sijawahi kuona haya wakati tuna milima sana? kumbe hata sisi udongo wetu ni hivyo hivyo.
Jamani hiyo comment ya kwanza imenisikitisha sana...haya mambo ya kuzima simu usiku sio mazuri. Hata mimi nilishafiwa walinipigia simu usiku mzima hawanipati simu zote nilikua nimezima. Lakini toka siku hiyo nimelearn my lesson. Simu za usiku wa manane zinashtua sana. na nyingine wala sio za misiba ni za wale wazembe fulani hata uwaeleze vipi tofauti ya masaa ya huku na Tanzania hawasikilizi. Wao watakupigia tu simu saa kumi asubuhi. halafu ukipokea tu utasikia ah kumbe umelala basi nitakutafuta baadaye....heeeee
Poleni sana