Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Haroun Ali Suleiman(kulia) akikabidhiwa vifaa vya shule na Mkurugenzi wa Vodacom Foundation Mwamvita Makamba(kushoto) kwa ajili ya wanafunzi wa shule ya sekondari Jang’ombe ambapo mfuko huo wa kusaidia jamii wa Vodacom ulikabidhi madarasa 12 katika shule hiyo waliyokarabati kwa thamani ya shilingi Milioni 24.

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Haroun Ali Suleiman (kulia) akiviangalia vifaa vya shule mara baada ya kukabidhiwa na Mkurugenzi wa Vodacom Foundation Mwamvita Makamba(kushoto)wakati huohuo Vodacom Foundation walikabidhi rasmi madarasa 12 waliyoyafanyia ukarabati katika shule hiyo ya sekondari Jang’ombe iliyopo Zanzibar,ukarabati huo uligharimu shilingi milioni 24.

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Haroun Ali Suleiman(kushoto) akiwasalimu baadhi ya Wanafunzi wa Jang’ombe sekondari iliyopo Zanzibar mara baada ya kukabidhi madarasa 12 katika shule hiyo yaliyokarabatiwa na Vodacom Foundation kwa thamani ya shilingi Milioni 24.
Mkurugenzi wa Vodacom Foundation Mwamvita Makamba akiongea na wanafunzi pamoja na uongozi wa shule ya sekondari ya Jang’ombe iliyopo zanzibar mara baada ya kukabidhi rasmi madarasa 12 kwa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Haroun Ali Suleiman,Madarasa hayo yaliyokarabati kwa thamani ya shilingi Milioni 24.
Baadhi ya Wanafunzi wa Sekondari ya Jang’ombe iliyopo Zanzibar wakiomba dua mara baada ya kupokea msaada wa madarasa 12 yaliyofanyiwa ukarabati kwa thamani ya shilingi milioni 24 na Mfuko wa kusaidia jamii wa Vodacom (Vodacom Foundation).







Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. Mwamvita,

    You just made my morning...You officially have the best job
    in the world!!! Your occupation has combined the highest passions in my life, style,travel and giving back to the community. I hope to one day see the world in the manner that you have done. As a guy I find your pics inspirational and challenging. You give me insight on places in TZ that I wish to see one day!

    Gosh! i'll says it, you are absolutely gorgeous, and your outfit just oozes class, style and grace. Love it (Hivi hao Voda wanakuwekea bajeti ya mavazi au?)

    -secret admirer from the other side

    xxx

    ReplyDelete
  2. Huu mdomo!! Du!!

    ReplyDelete
  3. Hongereni Vodafone, May GOD bless you all.
    Jamani wenye uwezo tujitolee kuchangia maendeleo ya nchi kwani serikali peke yake haiiwezi hiyo kazi ndio maana Mungu akawapa baadhi uwezo na wengine hawakupata huo uwezo.
    Ndugu zangu wa Jang'ombe mliwapa Vodafone zawadi ya Ngonjera au mliwabania maana kwa Ngonjera hamjambo.
    Mdau TUMEKUJA SCHOOL.

    ReplyDelete
  4. Mambo mazuri lakini kuna swali nauliza mnaomba dua huku wanawake wapo vichwa wazi (tehetehe) sijui labda dua za kizushi maana kifiqhi hamna kitu kama hicho

    ReplyDelete
  5. Baniani mbaya kiatu chake dawa, si munaona RA anavyogawa fedha zake bila ya kutaka kupigwa mapicha kama manyangumi!!!

    RA Admirer.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...