Suma Ngonyani
1955-2008


Leo Machi 24, 2010 ni miaka miwili kamili toka ulipotuaga, mpendwa wetu Suma. Tunakukumbuka na kukumiss sana.

Wewe ulikuwa mhimili wa maisha yetu na nguzo imara ya familia yetu, jamaa zetu na marafiki zetu.
Wewe ulikuwa mwangaza katika mihangaiko yetu. Ulikuwa nyota ya asubuhi katika maisha yetu. Wewe ulikuwa mshauri mwenye hekima kwa wote waliokusikia. Wewe mlezi maridhawa kwa wanao na sisi sote.
Wewe ulikuwa faraja na kitulizo kwa waliokuwa wakihangaika.
Wewe ulikuwa tabibu hodari kwa wenye maradhi, ukawatunza kwa upendo wagonjwa wa aina mbalimbali, ukawatia moyo waliozidiwa.
Ewe mkunga uliyehudhuria matukio mengi ya wageni kuingia duniani hapa, umo katika kumbukumbu zetu.

Unakumbukwa na familia huko Mbeya na Kiwira, kadhalika Mkongo-Namtumbo, bila kusahau Dar es Salaam na pande zote za Tanzania. Wapendwa wa Michigan na Marekani kwa jumla, na hata wale wa Yuropa wote wanakukumbuka sana.
Yote ni mapenzi yake Mwenyezi Mungu.

Na ahimidiwe leo na milele kwa maana yeye alitupa wewe kama zawadi kwetu. Tumeifurahia dunia kwa sababu ya zawadi hiyo.

Tembelea ukurasa wa kumbukumbu
http://suma-ngonyani.virtual-memorials.com/
main.php?action=reflections&mem_id=16310

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. KYALA GWA MAKA!NDAGA SEMEKI!

    ReplyDelete
  2. with all due respect to the late Suma as my heart goes to the family and friends, is it me or just my english that tumekukumbuka is the same as tumekumiss?? mmmh.

    ReplyDelete
  3. REST IN PIECE MAMA!

    ReplyDelete
  4. Mwenyezi akupokee kwenye makao yake ya milele, AMINA!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...