Kiongozi wa msafara wa mashabiki wa soka wanaolekea afrika ya kusini kushuhudia kombe la dunia Bw. John Inden [katikati]akiwa ndani ya kreta ya mamlaka ya hifadhi ya ngorongoro[ncaa] mara baada ya kucheza soka la kuhamasisha na wenyeji wa eneo kutoka kushoto ni kijana wa jamii wa wafugaji wa kimasai leboi meeshaa,meneja wa uhusiano wa ncaa adam akyoo na mkurugenzi wa masoko wa bodi ya utalii nchini.
Msafara wa mashabiki wa soka kutoka ujerumani wanaolekea afrika ya kusini kushuhudia kombe la dunia john inden juu kreta ya mamlaka ya hifadhi ya ngorongoro[ncaa] mara baada ya kucheza soka la kuhamasisha na wenyeji wa eneo kufanyika kwa michuano hiyo barani afrika wakiwa na baadhi ya maofisa wa bodi ya utalii nchini[TTB] na ncaa. Picha na Woinde Shizza

Na Woinde Shizza,
Ngorongoro

Ikiwa zimebaki siku chache kabla ya kuanza kwa michuano ya soka ya kombe la dunia makundi ya mashabiki wanaelekea katika fainali hizo nchini afrika ya kusini kutoka ujeruamni na uholanzi yameingia nchini na kucheza soka na jamii mbalimbali katika maeneo ya Ngorongoro

Mashabiki wa kwanza walikuwa Wajerumani wapatao 32 wanaopita nchi sita za Afrika kwa njia ya barabara likielekea Afrika ya kusini lilifuatiwa na kundi la wadachi 120 kutoka uholanzi ambao walipiga soka ndani ya bonde la Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro na wenyeji vijana wa jamii ya Kimasai

Awali mashabiki hao walichezaa michezo kadhaa na vijana wa kimasaiwa Namanga wilayani Longido ambapo vijana wa kimasai walibuka na ushindi kwa kuwafunga Ujerumani mabao 2 kwa 1

Katika mchezo mwingine uKundi hilo licheza na Timu ya Wazee wa Kimasai wa Ngorongoro ambapo Timu hizo zilitoshana nguvu kwa kwenda sare ya bila kufungana mabao

Kiongozi wa Ujeruman Tobias Remberg alieleza wanahamasisha ufanyikaji wa michuano hiyo kwa mara ya kwanza barani Afrika

Meneja uhusiano wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro Adam Akyoo alisema kuwa kutokana na ukubwa wa tukio la kombe la dunia misafara hiyo imepewa kipaumbele kwa kuwezeshwa kufanya mazoezi katika maeneo hayo na pia kucheza mpira na wenyeji

Jana walitarajiwa kucheza michezo kadhaa katika mji mdogo wa Mto wa mbu wilayani Monduli kabla ya kuondoka kuelekea nchini Malawi.

Wajerumani hao wanapita katika nchi sita za Afrika ambazo ni pamoja na Misri,Kenya,Tanzania,Kenya,Zambia,Botswana na kuingia Afrika ya Kusini

Walianza safari yao mjini Hamburg nchini Ujerumani na kupita,Italia, Austria na kuingia Afrika kupitia Misri ambapo litawasili Johannesburg Afrika ya Kusini siku moja kabla ya kuanza kwa mashindano hayo ya Kombe la Dunia Juni 11, mwaka huu.

Mashabiki wa uholanzi nao walianza safari yao Amsterdam wakiwa katika msafara wa watu 120



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 26, 2010

    Kaka Issa,

    This is the lost opportunity, We would have more tourists flocking to our country following World Cup, if we would have put mechanism in place that would allow these people to bring in much needed money to our country.

    We should have created RADIO and TV ADDS, on the various local networks here in EUROPE.

    The Ambassodors should put their voices/messages on local RADIO accross EUROPEAN countries, there are a lot of people here are listening to radios.

    Yesterday when, I was driving home, I hear a KENYAN ambassador thumping up for tourists to come to KENYA, but we remain quite following up this world cup.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...