SAFARI SIYO KIFO

Kikosi cha Akudo Impact

BENDI ya Muziki ya dansi ya Akudo Impact Wanapekecha Pekesha Ijumaa ya Julai 9 itafanya utambulisho rasmi wa Albamu mpya na utambulisho wa wanenguaji wake wapya utakafanyika kwenye Ukumbi wa Polisi Jamii Uliopo Dodoma .

Mratibu wa onesho hilo hilo Zahor Said, amesema kuwa onesho hilo pia litakuwa na utambulisho wa albamu inayotwa 'History No Change', pamoja na wanenguaji wapya ambao wametoka nchini Congo .

Said alisema kuwa onesho hilo maalum litaaanza saa 2 usiku nia ni kuwapa burudani wapenzi wa mkoa wa dodoma na vitongoji vyake.

“Tumejipanga kutoa burudani siku hiyo maalum ya utambulisho Akudo itafanya vitu vya uhakika itatoa vionjo vya wanenguaji wapya ambao Akudo imewachukuwa kutoka Congo ,”alisema Said.

Said alisema katika utambulisho huo kutakuwa na burudani nyingine mbili ambazo zitasindikiza usiku huo ambapo mazungumzo na bendi hizo yanaendelea.

Baadhi ya nyimbo za albamu hiyo ni Ndoa, Umefulia na Ubinafsi na inayobeba albamu hiyo History No Change.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. JACK PEMBAJune 26, 2010

    HII BULOGU NI YA WATU WENYE NAZO TU HASA WALE WALIOSOME MUZUMBE CHUO KIKUU CHA UNIVESITY CHA KULE MOLOGOLO. SASA WADAU WAKUU WA HII JAMVINI NI

    JOHN MASHAKA
    RIDHIWANI KIKWETE
    JACK PEMBA
    PAULO KAMAU (ANAKUJA NA BRIFIKESI)

    SISI WAKULIMA HATA KAMA TUMESOMA MUZUMBE LAKINI HATUKUBALIKI KWA MAANA HATUNA DAU. NI WENYE DAU TU, AMBAYO SIYO VIZURI.ANAKL HATA SISI HATUNA DAU ILA ITAKUWA VIZURI UKIWEKA NYIMBO ZETU, TUMEIMBWA NA WANAFUNZI WA CHUO CHA MUZUUMBE

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 26, 2010

    Kweli sasa wadau tumetambua kuwa Globu ya Jamii pia ni PRESS CONFERENCE YA JAMII a.k.a Speakers'corner(go to public speaking history www.speakerscorner.net ya London's Hyde Park), wadau hiki ni kiwanja chetu.

    Mdau
    Honolulu, Visiwani Pasifiki.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...