JK akihutubia katika mkutano huo leo
JK akisalimiana na baadhi ya wanachama wa CCM, Mkoa wa Dar es Salaam waliojitokeza kumdhamini katika fomu za kuomba kuteuliwa kugombea Urais, leo kwenye Ukumbi wa Ubungo Plaza, Dar es Salaam.Ridhiwani Kikwete (wa pili kushoto) ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Vijana waliopewa jukumu la kuratibu shughuli ya kutafuta katika mikoa kumi wanachama wa Chama Cha Mapinduzi wa kumdhamini Mwenyekiti wa Taifa wa CCM, Rais Jakaya Kikwete katika fomu za kuomba kuteuliwa kugombea Urais, akijadiliana jambo na baadhi ya vijana wa chama hicho.
Baadhi ya wanachama wa CCM, Mkoa wa Dar es Salaam, wakimshangilia JK (hayupo pichani) wakati akiingia kwenye ukumbi wa Ubungo Plaza jana,kuzungumza na wanachama 350 waliojitokeza kumdhamini kwa kujaza fomu za kuomba kuteuliwa kugombea Urais, leo kwenye Ukumbi wa Ubungo Plaza, Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 7 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 25, 2010

    WEWE CCM TU mwandishi yatakiwa uwe kotekote MR TWO achukua card ya chadema iyo vipi?

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 25, 2010

    tz kwa kupoteza hela haijambo!! sasa hizo t-shirts za nini? kwani watu wakienda kwenye mkutano wa CCM bila kuvaa sare hautafanyika. nchi tajiri duniani hazifanyi huu upuuzi. hivi mliona jinsi uchaguzi wa UK ulivyokua?watu wanapiga nguo zao kawaida,kinachoongea ni sera na sio sare!!kha.. badilikeni jamani. hizo hela mngenunua dawa na kuzisambaza kwenye mahospitali yetu..

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 26, 2010

    NA BADO MTAJIBEBA MWAKA HUU!!

    Mbona nyie mnavaa magwanda ya Mgambo ya khaki na hakuna mtu anapiga kelelee!

    CCM OYEE! KIKWETE OYEEE!!

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 26, 2010

    wanaoaidia pesa za kampeni inatakiwa ijulikane vyanzo vya pesa zao, sio wanatuibia alafu wanajifanya kutoa msaada.alafu na mimi sioni mantik ya kuvaa sare,muda wote huwa tunaangalia kubana matumizi.sio eti kwa sababu hawa wamevaa kaki basi sie tuvae njano na wale wavae kijani...alafu kuna sura za wagombea hazibadilikagi tangia 95, elimu bado hatujaiweka katika matumizi..mfano mheshimiwa lipumba kwani lazima ugombee wewe??

    ReplyDelete
  5. SANGU SECONDARY OYEEE!June 26, 2010

    WE BWANA MDOGO SAID NTIMIZI HEBU FANYA MAZOEZI EBOO!UTAPASUKA MTOTO ULIKUWA UNA SURA YA MAMA BONGE LA HANDSOME CHEKI SASA ULIVYOCHAKAA,PUNGUZA MWILI DOGO,SISI KAKA ZAKO WA SANGU SECONDARY TUMECHUKUA HATUA YA KUKUPA USHAURI NA SIKU ZOTE MANENO YA MKUBWA HAYADONDOKI HIVYO TUNATUMAINI UTAYAPOKEA KWA MIKONO MIWILI.

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 26, 2010

    anony namba 2 nakuunga mkono; tumechoshwa na sare sasa tunataka sera.
    chadema hoyee.

    ReplyDelete
  7. AnonymousJune 26, 2010

    nguo bure hizo wathamini wa dosi !!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...