

UHUSIANO KATI YA SWAHILI NA
MOZAMBIQUE FASHION WEEK WAIMARIKA
Ni awamu ya sita kwa tamasha kubwa la kila mwaka Mozambique fashion week litakalofanyika kuanzia tarehe 6-11 Disemba mjini Maputo Msumbiji. Mahusiano kati ya Swahili na Mozambique fashion week yalianza mwaka 2009 kwa washiriki Adelia na Sheila Tique kuiwakilisha Msumbiji katika Swahili fashion week 2009 na baadaye Swahili fashion week iliwakilishwa na Jamira Vera Swai.
“Mwaka huu Marinella Rodriguez aliiwakilisha Mozambique Fashion Week katika Swahili fashion week, kwa heshima na furaha kubwa tunajivunia kumchagua Manju Msitta kuiwakilisha Swahili fashion week katika tukio muhimu mjini Maputo siku ya tarehe 11 Disemba” alisema Mustafa Hassanali muanzilishi wa Swahili Fashion Week.
“Ni furaha kubwa kuiwakilisha Tanzania na Swahili fashion week katika maonesho ya Mozambique Fashion Week mwaka huu. Nina imani nitaipeperusha vizuri bendera ya Tanzania na Afrika mashariki katika tukio hili la kidunia.” Alisema Manju msita
Manju alichaguliwa na muandaaji wa maonesho ya mavazi wa kimataifa Jan Malan Umzingeli kwa kushirikiana na Swahili Fashion Week kwa kigezo kwamba kazi zake zina kiwango cha juu kulingana na ubora wa ubunifu wa mavazi yake.
“Huu ni mwanzo wa kuimarisha mahusiano baina yetu, na sio siasa pekee inayotuunganisha Tanzania na Msumbiji ila kupitia Utamaduni pia unatuunganisha.Uhusiano huu uendelee zaidi na kuwa imara mwaka hadi mwaka.” aliongeza Hassanali.
Ni awamu ya sita kwa tamasha kubwa la kila mwaka Mozambique fashion week litakalofanyika kuanzia tarehe 6-11 Disemba mjini Maputo Msumbiji. Mahusiano kati ya Swahili na Mozambique fashion week yalianza mwaka 2009 kwa washiriki Adelia na Sheila Tique kuiwakilisha Msumbiji katika Swahili fashion week 2009 na baadaye Swahili fashion week iliwakilishwa na Jamira Vera Swai.
“Mwaka huu Marinella Rodriguez aliiwakilisha Mozambique Fashion Week katika Swahili fashion week, kwa heshima na furaha kubwa tunajivunia kumchagua Manju Msitta kuiwakilisha Swahili fashion week katika tukio muhimu mjini Maputo siku ya tarehe 11 Disemba” alisema Mustafa Hassanali muanzilishi wa Swahili Fashion Week.
“Ni furaha kubwa kuiwakilisha Tanzania na Swahili fashion week katika maonesho ya Mozambique Fashion Week mwaka huu. Nina imani nitaipeperusha vizuri bendera ya Tanzania na Afrika mashariki katika tukio hili la kidunia.” Alisema Manju msita
Manju alichaguliwa na muandaaji wa maonesho ya mavazi wa kimataifa Jan Malan Umzingeli kwa kushirikiana na Swahili Fashion Week kwa kigezo kwamba kazi zake zina kiwango cha juu kulingana na ubora wa ubunifu wa mavazi yake.
“Huu ni mwanzo wa kuimarisha mahusiano baina yetu, na sio siasa pekee inayotuunganisha Tanzania na Msumbiji ila kupitia Utamaduni pia unatuunganisha.Uhusiano huu uendelee zaidi na kuwa imara mwaka hadi mwaka.” aliongeza Hassanali.
All the best Manju. Enjoy Maputo!
ReplyDeleteMteja Sugu!