Na Mwandishi Wetu

WALINZI wa Kampuni ya KK Security wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni kujibu shitaka la kuvunja godauni la Kampuni ya Tanzania Distilleries
Litimed.

Ilidaiwa mahakamani hapo juzi kuwa washitakiwa wote kwa pamoja walivunja godauni la kampuni hiyo na kuiba vinywaji vya aina mbalimbali vinavyotengenezwa katika kampuni hiyo.

Watuhumiwa hao ni Ezekiel John (22), Hamisi Mustapha (27) na James Shetta (21).

Mbele ya Hakimu Issa Kasailo, ilidaiwa na Mwendesha Mashitaka Inspekta wa Polisi, Mtani Magoma kuwa Novemba 2010, usiku eneo la Ubungo Millenium Business Park, washitakiwa walivunja godauni lililokuwa na vinywaji vya aina mbalimbali vyenye thamani ya sh. 36,186,042 mali ya kampuni ya konyagi.

Awali, washitakiwa hao walifutiwa kesi yao chini ya kifungu cha sheria cha 225,lakini hata hivyo Wakili wa Serikali, Hellen Moshi aliwakamata tena ili kuhojiwa upya, kesi ianze tena.

Hakimu alifuta kesi kwa sababu shahidi ambaye ndiye mpelelezi wa kesi hiyo alikuwa hakufika mahakamani hapo.

Hata hivyo, washitakiwa hao walikana mashitaka na kurudishwa rumande hadi kesi hiyo itakapotajwa tena Juni 4 mwaka huu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 25, 2011

    wafanyakazi wa hii kampuni wanashirikiana sana na wakubwa kuiba mizigo kwenye makontena bandarini,kuna kesi zipo mahakamani lakini haziishi,sababu wanaoneana aibu

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...