KATIBU wa NEC, Itikadi na Uenezi CCM, Nape Nnauye, akitia saini kitabu cha maombolezo ya kifo cha Nontsikelelo Sisulu, aliyekuwa mke wa mpigania uhuru wa Afrika Kusini, marehemu Walter Sisulu,katika Ubalozi wa Afrika Kusini mjini Dar es Salaam.

NA MWANDISHI WETU

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimetoa pole kwa chama cha ANC, kufuatia kifo cha Mama Nontsikelelo Sisulu, mke wa aliyekuwa mpigania uhuru wa Afrika Kusini, Walter Sisulu.

Akuzungumza baada ya kutia saini kitabu cha maombolezo ya kifo hicho, kwenye Ubalozi wa Afrika Kusini mjini Dar es Salaam,Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye alisema, CCM imeguswa na kifo hicho kwa sababu mbali na kuwa mke wa mpigania uhuru, Mama Sisulu alikuwa mstari wa mbele kupigania haki na usawa wa binadamu.

Nape alisema, katika uhai wake, Mama Sisulu alitumia taaluma yake ya uuguzi kuwafundisha wauguzi wenzake ambao walihudumua wanaharakati waliokuwa katika mapambano ya kusaka uhuru wa Afrika Kusini.

Alisema, Mama sisulu atabaki kuwa mfano wa wapenda usawa wa binadamu duniani kwa sababu hata baada ya Afrika Kusini kupata uhuru, alikuwa miongoni mwa viongozi waliosimamia maridhiano ya kusahau madhila yaliyofanywa baina ya makaburu na raia wa Afrika kusini kabla ya uhuru.

Nape alisema, licha ya ukatili na ubaguzi wa rangi waliokuwa wakiufanya makaburu, lakini maelewano yaliyofanyika baada ya uhuru wa chini ya wanaharakati akiwemo Mama Sisulu wazungu hawakubaguliwa. Alisema matendo ya Mama Sisulu yatabakia kuwa mfano bora kwa wapinga ubaguzi na wapenda amani duniani ikiwemo Tanzania.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...