Mh. Kalonzo Musyoka, Makamu wa Rais wa Kenya akipokea maelezo juu ya bidhaa za aina mbalimbali zinazotengenezwa Tanzania










Na Mwandishi wetu, Nairobi
Mataifa ya Afrika ambayo yana uwakilishi hapa Nairobi, kwa pamoja yaliandhimisha siku ya Afrika tarehe 25 Mei, 2011 sherehe ambazo zilifanyika katika ofisi za Uwakilishi wa Serikali ya Kenya katika Umoja wa Mataifa (Kenya Mission to UNON).  

Haya ni maadhimisho ya 48 tangu kuazishwa kwa siku hii, ambapo kimsingi mataifa ya Afrika hutumia siku hii kama  njia mojawapo ya kutathmini mafanikio ambayo yameweza kufikiwa katika Nyanja mbalimbali.

Makamu wa Rais wa Kenya akiangalia kwa makini wine za Tanzania kama vile Rosier, Rose Wine ambayo inatengenezwa na CETAWICO LTD, Dodoma, G. MERLINI WINE ambayo inatengenezwa ma Missionaries of the Precious Blood, Miyuji Dodoma, Tanganyika vineyards – Dodoma, Dompo Red wine  kutoka Alko Vintages Dodoma, Annunciata Sweet white Grape wine, inayotengenezwa na Missionaries of the Precious Blood, Miyuji, Dodoma, Buffalo wine na Rhino.
Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo alikuwa Mh. Kalaozo Musyoka, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Kenya. Kauli mbiu ya mwaka huu katika kuadhimisha siku ya Umoja wa Afrika 2011 ni kuhamasisha na kuwawezesha vijana  kwa ajili ya maendeleo endelevu.

Maadhimisho ya siku ya Umoja wa Afrika yalienda sambamba na maonyesho ambapo kila nchi ilipata fursa ya kuonesha vitu mbalimbali.
Mmoja wa wageni akipokea maelezo
kutoka kwa Bibi Joy Njelango
Katika maonesho hayo banda la Tanzania ambalo siku hiyo lilitia fora liliratibiwa ipasavyo na Ubalozi wa Tanzania  Nairobi na lilisheheni bidhaa mbalimbali ambazo zinatengenezwa nchini Tanzania.  

Bidhaa ambazo zilionyeshwa ni pamoja na hizi zifuatazo:
Mgeni akiwa kavutiwa na Dodoma Wine
          (1)     Kahawa
(2)     Majani ya chai ya aina mbalimbali kama vile African Pride, Chai Bora, Green Lebel, Kilimanjaro, Simba chai.
Kina mama wakiongozwaa na Kaimu Balozi Bi Grace Mgovano (wa pili kulia) wakipamba Banda la Tanzania ipasavyo.Hii ilikuwa ndiyo sare ambayo iliacha wageni wengi hoi bin taaban. Ndiyo Bandaa pekee ambalo lilikuwa na sare kama inavyoonekana pichani.
(3)     Wine za aina mbalimbali kama vile Rosier, Rose Wine ambayo inatengenezwa na CETAWICO LTD, Dodoma, G. MERLINI WINE ambayo inatengenezwa ma Missionaries of the Precious Blood, Miyuji Dodoma, Tanganyika vineyards – Dodoma, Dompo Red wine  kutoka Alko Vintages Dodoma, Annunciata Sweet white Grape wine, inayotengenezwa na Missionaries of the Precious Blood, Miyuji, Dodoma, Buffalo wine na Rhino.
(4)     Konyagi
Wageni kibao walitembelea banda letu
(5)     Khanga, Batiki, na nguo zilizoshonwa kwa kutumia khanga na batiki ambazo zilipatikana kutoka Mitindo House Dar es salaam.
(6)     Mbuzi ya kukunia nazi pamoja na nazi.

Kikosi kazi cha Ubalozi wetu Nairobi
Kimsingi Banda la Tanzania lilipata mvuto mkubwa na wengi walionyesha wazi kupenda wine ya Watanzania japo wageni wengi walionyesha wazi kutokuwa na taarifa kwamba Tanzania pia inatengeneza wine.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...