Familia ya marehemu JULIA JOHN IVAMBI inapenda kutoa shukurani za dhati kwa ndugu, jamaa na marafiki wote kwa kufanikisha msiba wa mama yao mpendwa uliotokea tarehe 11/11/2011 katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar-Es-Salaam.
Na baadae kuzikwa Kondoa mkoani Dodoma siku ya tarehe 15/11/2011.
Tunapenda pia kuwakaribisha katika mkesha wa kumalizia msiba utakaofanyika nyumbani kwa marehemu Mburahati NHC ‘B’ nyumba namba 540 siku ya ijumaa kuanzia saa 12 jioni tarehe 23/12/2011 hadi jumamosi mchana. Kufika kwako ndio mafanikio ya shughuli hii.
BWANA AMETOA, BWANA AMETWAA. JINA LA BWANA LIHIMIDIWE.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...