Mkuu wa kitengo cha habari na mawasiliano katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bw. Assah Mwambene akiwa kapiga chunlai yenye rangi ya bendera ya Taifa. Bila shaka vazi hilo ni juhudi binafsi za wabunifu katika kuendeleza libeneke la msako wa Vazi la Taifa ambao mchakato wake umeanza

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 29 mpaka sasa

  1. ubunifu mzuri, ila kwanini watanzania hatujui mpangilio wa rangi za bendera ya taifa letu?

    ReplyDelete
  2. Hapo sawa ila amekosea blue kuiweka juu, nashauri blue iwekwe chini badala ya yellow

    ReplyDelete
  3. Hii ni nzuri, lakini wasiwasi wangu ni kuwa, hizo rangi zilizo tumika zimekuwa na mrengo wa chama fulani, na kwa mujibu wa waraka wa umma kuhusu mavazi yanayo takiwa kuvaliwa kunako sehemu za kazi, ni vizuri yasiegemee kwenye mrengo wa Chama chochote cha Siasa.

    Ushauri wangu vema yakafanyika marekebisho ili yaweze kuvaliwa sehemu za Kazi kama ofisi za Serikali.

    ReplyDelete
  4. Uchafu mtupu...

    ReplyDelete
  5. bayaa kwani lazima liwe na bendera ya taifa walau mngechukua rangi mbili hapo blue na kijani. sasa mambo ya kuvaa bendera hapana kwa kweli... na wee mzee wa kubana na koleo hamna kubana hii meseji, huu ni mtazamo wangu.

    ReplyDelete
  6. HILI NI VAZI LA CCM SIO TAIFA.... MAIN COLOR KABADILISHE...THAT GREEN STINKS

    ReplyDelete
  7. nzuri lakini nadhani blue iwe chini ya ufito wa njano na sio kama hivyo ilivyo sasa

    ReplyDelete
  8. hebu ngoja niwaulize, kwani vazi la taifa lazima liwe na rangi za bendera? mbona nikiwaangalia Wajapan, wa Ghana, Waganda wana mavazi yao ya taifa lakini hayana marangi ya bendera zao? wabunifu hebu kuweni wabunifu bila kuweka hizo rangi please

    ReplyDelete
  9. KAMA VILE UMEIBA BENDERA NA KUISHONA SHATI HAIFAI HATA KIDOGO. HAPA UBUNIFU BADO.

    ReplyDelete
  10. Vazi la taifa ni vizuri liwe zuri na linalopendwa na wavaaji. La sivyo mnapoteza muda bure. Kizuri chajiuza kibaya chajitembeza.

    Wanaotafuta vazi watumie ubunifu, akili, maarifa.

    Akili za kijasiri amali ndio zitumike siyo za kijamaa

    ReplyDelete
  11. Kazi kwelikweli kama vazi la Taifa ndio hili au liwe bendera. Kunahatari hata kukosekana kwa heshima ya bendera au kuabudiwa kwa vazi hilo.Ubunifu huu haufai endeleeni kuumiza vichwa kwanza sio kukurupuka.

    ReplyDelete
  12. kwa nini wa2 sio wabunifu?kwani lazima vazi la taifa liwe na bendera ya taifa hebu wa2 wajitahidi kufikiri zaidi.

    ReplyDelete
  13. National dress:
    What is a national dress? http://en.wikipedia.org/wiki/Folk_costume
    Reading wikipedia and some other sites the only conclusion I can come to is maybe the committee should be concentrating on more pressing issues like finding ways to raise funds within our society for projects such as clean water in the villages, affordable housing for the masses, dispersing management knowledge for small scale business. I can go on and on with areas such committee (which will take up the tax payers’ money) can be of service.
    The issue I have with the traditional dress is vast because I don’t have answers to the following:
    Who is a Tanzania?
    What is the cultural make up of Tanzania and will it be reflected in the traditional dress??
    Looking at Wikipedia, Kanzu is considered a traditional dress; well I wonder what we wore before the Arabs came to town.
    What impact, if any, will this traditional dress play in the future for our nation?
    Will it be ‘ooooh okay’ and life moves on?
    50 years have gone and we are still stuck up in committees that don’t solve the everyday problems our people are facing!!
    Does a mother who has to walk 10kms to fetch water from well give a hoot if there is a national dress or not?? Give her running water near her house and she will push the wheel of development even further than she has so far!
    We need to change the way we do things and its only ourselves who can do it. When we as individuals can galvanize creativity, the Government will take us more serious and respect our vote and taxes!

    ReplyDelete
  14. Hiyo mbona ni vazi la timu ya yanga. Wanasimba hatuwezi nunua ng'o!

    ReplyDelete
  15. Naungana na anony Wed Dec 14, 10:11:00 AM 2011. Kwani vazi la taifa mpaka liwe rangi za bendera ya taifa? Halafu vazi la taifa linapaswa kuwa 'full', yaana juu mpaka chini, sio shati au suruali pekee. Tujitahidi kuwa wabunifu zaidi ya hapa.

    ReplyDelete
  16. Haya mambo ya vazi la taifa tumeshachelewa sana. Ilibidi vazi la taifa libuniwe mara tu baada ya kupata uhuru sio kusuburi miaka 50 baadae. Ilikuwa rahisi kufanya hivyo enzi ya chamna kimoja kwani vazi lingebuniwa na chama kingeamua kuwa hilo ndilo liwe vazi la taifa. Hakuna mtu angebisha au kuleta malumbano. Hili sidhani kama linawezekana enzi hizi za utandawazi na uhuru wa kuchagua.

    ReplyDelete
  17. Kazi kweli kweli! Mbona wabongo tunakuwa wavivu wa kubuni? Suala hili linakuwa gumu kutokana na kupoteza Utamaduni wetu na kuiga utamaduni wa Kimagharibi.Wakiona Mmasai amevaa vazi lake la asili wanakebehi au Mzaramo akicheza Ngoma anaonekana amepitwa na wakati!Lakini mwana Hip hop akipanda Jukwaani huku akifuata sauti yake kutoka ktk CD na kuwaambia watu "PIGA KELELEEEEE!" Watu wanatoa 20,000 fasta kusikiliza "PIGA KELELEEEEE" Mwanzo mwisho.

    ReplyDelete
  18. VAZI LA TAIFA SI KITU CHA MPAKA COMMITTEE IKAE BALI NI KITU KINACHOKUJA AUTOMATICALLY KWA WATU WENGI KUPENDELEA KUVAA NGUO ZA AINA FLANI (KAMA UTAMADUNI FLANI HIVI YAANI TUNAKUWA KAMA VILE WAMASAI WANAVYOVAA BASI NA SIE KTK WINGI WETU TUNAKUWA TUNA MAVAZI FLNI). NI NGUMU KWA TAIFA LA VIJANA WENGI WANAVAA MILEGEZO NA SKINI JEANS ALAFU TUSEME TUNALETA VAZI LA TAIFA, HAPA NAONA NI KAZI NZITI MFANO MZURI ONA VIJANA WANAVYOVAA HASA VYUONI ALAFU NDIO UTAPATA JIBU MAANA KAMA VYUONI WANAVAA HIVYO MAANA YAKE KWA ALIE MTAANI ATATEMBEA UCHI KABISA MAANA ROLE MODEL AMBAO NI WANAVYUO WANAVAA KIHASARAHASARA

    ReplyDelete
  19. Aaaghhhhh huo mrangi wa KIJANI ndo soo lenyewe,SIVAI hata kwa MIKWAJU,hii rangi nikiiona tu basi mie nageuka ghafla,kama nilikua naangalia tv basi hujikuta tu nisha bonya kitufe.

    ReplyDelete
  20. WABUNIFU NA WAVAAJI WOTE VIPOFU.

    ReplyDelete
  21. VAZI LA TAIFA::::

    Wengi wamefurukuta lakini wazo la kuingiza angalau vionjo vya Mgolole na Lubega havipo kabisa kwa Wabunifu wa vazi la taifa!

    Ingawa picha nyingi za historia ya watu wa zamani zimeonyesha wakiwa ktk vazi hilo ,ingefaa wabunifu waanzie hapo na kuendela mbele ili kupata kitu sahihi.

    ReplyDelete
  22. Hilo lirangi la kijani hakifai, HILO NI VAZI LA CCM. AGGRRR!!!

    ReplyDelete
  23. Kwani vipi?

    Pana tofauti gani kubwa ya rangi za Bendera ya CCM na rangi za Bendera ya TAIFA?

    HEBU TUBISHANE KWA HOJA ZA KISAYANSI KAMA HAPA CHINI:
    ___________________________________
    (Experiment)
    ___________________________________
    BENDERA YA TAIFA:-
    -Nyeusi
    -Bluu
    -Kijani
    -Njano
    -Nyeupe(ktk fito)

    BENDERA YA CCM:-
    -Kijani
    -Njano
    ___________________________________
    (Results)
    ___________________________________
    Rangi za CCM zimezaliwa kutokea Bendera ya Taifa!

    Mtu unaweza kuthubutu,kujaribu kumkana baba mzazi, lakini mama mzazi hakuna wa kusingiziwa!

    Sasa mnabisha nini?, mna akili kweli?...hamjui kuwa CCM ndio SERIKALI YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA?

    ReplyDelete
  24. Wajameni kutokana na Experiment nzito ya Kisayansi na ulinganishi iliyoshushwa na Profesa wa Vitendo hapo juu Mdau wa 24, Kuhusu rangi za nchi kwa kweli asiyeamini jarobio hilo la Sayansi na matokeo hayo ya Sayansi atakuwa si mwenzetu na atakuwa ni mchawi!

    ReplyDelete
  25. hilo alilovaa jamaa ni vazi la ccm lenye bendera PINDU ya taifa. yaani ameitukana bendera ya Tanzania kwa kuigeuza chini-juu!

    ReplyDelete
  26. VAZI LA TAIFA??? RIDICULOUS....!!! LET US THINK TWICE...!!!

    ReplyDelete
  27. Nashauri wabunifu wapewe nafasi ya kutoa mishono ambayo itawakilisha vazi la taifa.Watu hawataki kuchaguliwa rangi za kuvaa,kinachotakiwa ni mshono tu tofauti na hapo tutavaa uniform nchi nzima.

    ReplyDelete
  28. Nashauri wabunifu wapewe nafasi ya kutoa mishono ambayo itawakilisha vazi la taifa.Watu hawataki kuchaguliwa rangi za kuvaa,kinachotakiwa ni mshono tu tofauti na hapo tutavaa uniform nchi nzima.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...