Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano wa Vodacom Tanzania Rukia Mtingwa (kulia) akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) kabla ya kuchezesha droo ya kwanza ya mwezi kupitia promosheni ya M-pesa ili kupata mshindi wa shilingi Milioni kumi, wa pili kulia ni Afisa Masoko wa M-pesa Reenu Verma, na Meneja wa Mifumo ya kompyuta Bw. Patrick Makungu pamoja na mwakilishi wa Bodi ya michezo ya kubahatisha Tanzania bi. Chiku Saleh.
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano wa Kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania Rukia Mtingwa akipata taarifa kutoka kwa Askari wa upelezi Peter James Kilalo (38) aliebahatika kujishindia kiasi cha shilingi milioni kumi mara baada ya droo ya kwanza ya mwezi kupitia promosheni ya M-pesa kuchezeshwa katika Makao makuu ya kampuni hiyo jijijni.
Mkuu wa Kitengo cha Mifumo ya Kompyuta kutoka kampuni ya Simu za Mkononi ya Vodacom Tanzania bw. Josephat Kyando akimsikiliza kwa makini Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano Rukia Mtingwa wakati wa kuchezesha droo ya kwanza ya mwezi kupitia promosheni ya M-pesa ili kupata mshindi wa shilingi milioni kumi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...