Mtanzania mwenzetu aliyelazwa Washington Hospital nchini Marekani chumba # 2H22 hali yake bado sio nzuri na bado yupo ICU ambapo hawezi kuongea wala hatambui mtu yeyote ame,lala tu, Tunaomba mzidi kumuombea apate nafuu.
Tumeongea na Allis Kibwere ambae pale Hospitali anajulikana kama binamu wa mgonjwa na amesema ameisha wajulisha ndugu wa mgojwa wakiwemo watoto wake wawili waliopo Tanzania, akiongezea kuwa mgonjwa wetu amepatwa na pneumonia (nimonia), ambayo huchukua wiki moja mpaka tatu kwaa mgojwa wa aina hii kuweza kupata nafuu.
Kwa maelezo zaidi wasiliana na Ndugu Kibwere au unaweza kupiga Washington Hospital omba kuzungumuza na 2H au kwa Sandra Walsh ambae ni Assistant Nursing Director.
Asante.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...