Meneja Masoko wa Kampuni ya Bia Tanzania,Fimbo Butallah akimkabidhi zawadi Mtoto Abou Makame alieibuka mshindi wa kwanza wa kuimba nyimbo za muziki wa kufoka foka (Hip Hop) katika hitimisho la Tamasha la Wazi la Filamu nchini lililokuwa limedhaminiwa na Kampuni hiyo kupitia kinywaji chake kisicho na kilevi cha Grand Malt.Tamasha hilo limemalizika mwishoni mwa wiki hii.Kulia ni Mkurugenzi wa Sofia Productions ambao ndio walioandaa Tamasha hilo la Wazi la Filamu,Mussa Kisoky.
Meneja Masoko wa Kampuni ya Bia Tanzania,Fimbo Butallah na Mkurugenzi wa Kampuni ya Sofia Productions ambao ndio walioandaa Tamasha hilo la Wazi la Filamu,Mussa Kisoky wakiwa pamoja na Watoto waliotinga nne bora ya kusakata Dansi kwa watoto.
Wakazi wa Jiji la Tanga wakifatilia Burudani iliyokuwa ikitolewa na vijana wa Ice Cream Dances muda mfupi kabla ya kutangazwa kumalizika kwa Tamasha hilo la Wazi la Filamu nchini,lililokuwa likifanyika kwenye viwanja vya Tangamano,jijini Tanga.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 09, 2012

    Grand Malt wapigwe faini kubwa, kutumia watoto ni aibu and it is a criminal offence.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 09, 2012

    Hii grand malt ni kilevi ghafi, na sio kama si kilevi. Ni kama bia za kijarumani ambazo zao ni kama maji hazileweshi ukila kiasi. Ila ukifakamamia baadae zinalewesha.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...