Noti bandia zilizotua Iringa
Kamanda wa polisi wa mkoa wa Iringa Michael Kamuhanda akionyesha mfano wa noti za shilingi 10000 ambazo ni feki zilizokamatwa na jeshi la polisi zikiwa zinzonesha kuwa na thamani ya shilingi laki sabaNa Francis Godwin

Jeshi la polisi mkoa wa Iringa limetoa tahadhari kwa wananchi kuwa makani na fedha wanazolipwa ili kuepuka kubambikizwa noti bandia ambazo tayari jeshi hilo limekamata zaidi ya bandia zenye thamani ya zaidi ya shilingi 700,000.

Kamanda wa polisi wa mkoa wa Iringa Michael Kamuhanda amesema leo kuwa noti hizo zimekamatwa na askari polisi baada ya kupata taarifa kutoka kwa wananchi wasamaria wema.

Kamuhanda alisema kuwa hadi sasa jeshi hilo la polisi linawasaka wahusika wa mtandao huo wa kusambaza noti bandia katika mkoa wa Iringa ili kuchukuliwa hatua za kisheria.

Alisema kuwa fedha hizo ambazo zimekamatwa katika maeneo tofauti tofauti zina namba ambazo zinafanana na hivyo kuwataka wafanyabiashara na wakulima kuwa makini na watu wanaofika kununua mazao yao .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. FEDHA HALALI IMO MIKONONI MWETU!

    Wanyalu huko Iringa, ndugu zangu asalaleee, hakuna sababu ya kutoana damu sisi kwa sisi kwa fedha bandia na kurudishana nyumakimaisha na kimaendeleo.

    Nchi yetu ina mimali kibao na fursa lukuki za kuzichonga fwedha tena za halali kiulaini!!!

    Angalieni nchi yetu inakodolewa mimacho na hata majirani zetu, inagombewa kama mpira wa kona!

    Tazameni tunaburuzana na Malawi juu ya umiliki wa ziwa Nyasa, pia mmeona wandugu zetu Kenya wanavyolalamika kutaka kututumia Tanzania ki uchumi kama kimbilio la soko la ajira kwa watu wao.

    Zindukeni Wanyalu !!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...