Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya CRDB, Dk.
Charles Kimei akizungumza na waandishi wa habari wakati wa sherehe za Siku ya Familia ‘Familiy Day’ iliyofanyika
jijini Dar es Salaam na kuhusisha wafanyakazi wa benki
hiyo na familia zao.
Sehemu ya Burudani kwa Watoto.
DAR ES SALAAM, Tanzania
WATANZANIA wametakiwa kupanua wigo wa maendeleo yao
kiuchumi, ngazi ya mtu mmoja mmoja, familia na taifa, kwa kujiunga na kutumia ipasavyo
huduma ya ‘SimBanking’ inayotolewa na Benki ya CRDB
Hayo yalisemwa mwishoni mwa wiki na Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Dk Charles
Kimei, wakati wa sherehe za kila mwaka za Siku ya Familia ‘Family Day’ inayohusisha
wafanyakzi wa benki hiyo na familia zao, iliyofanyika kwenye Hoteli ya Kunduchi
Welt ‘n’ World’ jijini Dar es Salaam.
Alisema kuwa, kila mwaka wa sherehe hizo huwa na huduma moja
inayotangazwa, ambapo mwaka huu kipaumbele ni huduma ya ‘SimBanking’
iliyozinduliwa Aprili, ikiwa na lengo la kurahisisha maisha ya wateja na kuwapa
fursa ya kuachana na ukiritimba wa kupata huduma za benki kwa kupoteza muda
mwingi kwenye foleni.
Aliongeza kuwa, huduma hiyo ni ya kipekee miongoni mwa
mabenki nchini, inayoweza kuchangia upanuzi wa maendeleo ya kielimu, kiuchumi
na kijamii, kwa kumpa fursa mteja kuhamisha fedha kwenda akaunti yoyote ndani
ya mtandao wa CRDB.
“Huduma hii inasaidia huhamisha fedha kwenda kwenye simu ya
mkononi ya mtandao wowote nchini, kulipia ankara (bili) mbalimbali, kununua
muda wa maongezi kwa mitandao yote chini, kununua umeme wa LUKU, kutuma na
kuchukua fedha kwenye ATM bila kadi ya benki hata kama aliyetumiwa hana akaunti
ya benki hiyo,” alisema.
Akizungumzia sherehe hizo, Dk Kimei alisema kuwa ‘Family Day’
husaidia kuwaweka pamoja wafanyakazi na familia zao, ili kuzungumza, kujifunza,
kubadilishana mawazo, kuimarisha ushirikiano miongoni mwao, jambo ambalo
haliwezi kufanyika kirahisi kutokana na mgawanyiko wa matawi na ofisi zao.
Aidha, aliongeza kuwa, kwa miezi 11 ya mwaka huu wameweza
kuajiri zaidi ya wafanyakazi 700 na kufanya orodha ya waajiriwa katika benki
hiyo kuongezeka zaidi, ambapo ujazo wa faida kwa mwaka ukiwa ni asilimia 15,
huku akitarajia ongezeko la asilimia hizo kwa Desemba.
“Wastani wa miaka iliyotangulia ya ujazo wa faida ni
asilimia 18 hadi 20 kwa mwaka na kutokana na ukweli kuwa hii ni Novemba,
tunatarajia ongezo hilo kwa Desemba ili kufikia ama kuvuka kiwango cha miaka
iliyopita,” alisema.
nini maana ya kuasa? ametuasa au ametuhamasisha?
ReplyDelete