Mkurugenzi wa VETA nyanda za juu,Monica Mbele akiangalia moja ya darubini katika karakana ya vifaa tiba kwenye Hospitali ya St. Joseph Peramiho,wengine ni fundi mkuu wa karakana hiyo Baraka Chumbwi kushoto na katikati kaimu mganga mkuu wa mkoa wa Ruvuma Dkt Benedict Ngaiza.
Mkurugenzi wa Mamlaka ya elimu na mafunzo (VETA) nyanda za juu,Monica Mbele akiangalia moja ya vifaa tiba vilivyoharibika katika karakana ya Hospitali ya St Joseph Peramiho,Songea vijijini.VETA ina tarajia kufundisha wataalam na mafundi wa hospitali mbalimbali kutengeza vifaa vilivyoharibika ambapo itasaidia kuokoa kiasi kikubwa cha fedha kwa kuagiza au kuleta mafundi kutoka nje ya nchi kwa ajili ya ukarabati wa vifaa hivyo.
Mkurugenzi wa VETA nyanda za juu,Monica Mbele akiangalia mshine ya kufuria nguo ambayo imeharibika.
Kaimu mganga mkuu wa hospitali ya mkoa wa Ruvuma (homso) Dkt Benedict Ngaiza kulia na mkurugenzi wa VETA nyanda za juu,Monica Mbele wa pili kulia wakiangalia kiti kinachotumika kwa ajili ya shughuli za upasuaji katika hospitali ya St Joseph Peramiho jana.
Fundi mkuu wa karakana ya vifaa tiba katika hospitali ya st Joseph Peramiho Baraka Chumbwiakionesha mojawapo ya mshine ya kupiga picha kwa wataalam na mafundi kutoka chuo cha veta Songea,mafundi kutoka hospitali ya mkoa Ruvuma na ujumbe wa mamlaka ya elimu na mafunzo(veta)nyanda za juu ukiongozwa na mkurugenzi wake Monica Mbele.PICHA NA MUHIDIN AMRI - GLOBU YA JAMII,RUVUMA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...