Chief Technical Advisor Youth Entrepreneurship Facility and WED -ILO Bw. Jealous Chirove akizungumza wakati wa uzinduzi wa Wiki ya Kimataifa ya Wajasiriamali uliofanyika jijini Dar es Salaam ambapo amesema vijana lazima wawe na moyo wa kujituma na kuhakikisha wanapanua wigo wa kujiajiri wenyewe na kuondokana na fikra za kuajiriwa peke yake.
Aliongeza kuwa ujasiriamali katika nchini kama Tanzania ni mkombozi wa pekee katika tatizo la ajira hasa kwa vijana kwa kujiendeleza na mafunzo mbalimbali ya ujasiriamali kama njia pekee ya kujiajiri wenyewe.
Mwenyekiti wa Shirika Lisilo la Kiserikali la ZAYEE (Zanzibar Association for Youth Education and Empowerment) Bw. Masoud Salim Mohamed ambao ndio waandaaji wa maadhimisho ya wiki ya wajasiriamali inayoendea jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Shirika Lisilo la Kiserikali la ZAYEE (Zanzibar Association for Youth Education and Empowerment) Fatma Mabrouk Khamis akielezea jinsi alivyovutiwa kufanya maadhimisho ya Wiki ya Kimataifa ya Wajasiriamali hapa Tanzania ikiwa ni mara ya kwanza baada ya kuona yanavyofanyika nchini Marekani alikokwenda kujifunza juu ya ujasiriamali. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Professional Approach Group Modesta Mahiga akitoa nasaha zake kwa vijana mbalimbali kuhusu ujasiriamali faida na changamoto zake wakati wa maadhimisho ya wiki ya ujasiriamali hapa nchini.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Relim Entertaiment, Bi. Emelda Mwamanga Mtunga akizungumza wakati wa maadhimisho ya wiki ya ujasiriamali ambapo alitumia nafasi hiyo kuelezea uzoefu na changamoto za ujasirimali nchini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...