KATIKA kuelekea sikuu za Krismasi na Mwaka mpya pilika pilika
zimeongezeka katika mji wa Moshi na mkoa wa Kilimanjaro kwa ujumla
huku vibaka pia wakiendelea na udokozi na wizi wa vitu mbalimbali.
Katika kuthibitisha hilo juzi Tanzania Daima limeshuhudia mkazi wa
kijiji cha Nshara, Machame wilayani Hai,ambaye jina lake
halikupatikana mara moja amenusurika kuuawa kufuatia kipigo kutoka kwa
wananchi wenye hasira kumshambulia kwa silaha za jadi baada ya kuiba
kitoto cha nguruwe maarufu kama "Kiti moto".
Tukio hilo la aina yake ambalo linaashiria maandalizi ya siku kuu hizo
lilitokea juzi majira saa 5.30 asubuhi kijijini humo baada ya mkazi
huyo kuonekana akiwa amembeba mnyamya huyo begani akiwa katika
mfuko,maarufu kama Sandarusi mithili ya mzigo wa kawaida.
Akizungumzia tukio hilo,mkazi wa kijiji cha Nshara, Husein Mbaruku
alisema mtu huyo alionekana akinyata katika banda la Nguruwe akiwa na
mfuko wake akiamini kuwa hakuna mtu aliyemuona ingawa wenyeji nao
walikuwa wakimvizia ili kuona anachotaka kufanya.
"Huyu bwana ni mwizi mzoefu katika eneo hili ,mara kwa mara wenyeji
hapa wamekuwa wakilalamika kuibiwa nguruwe wao leo naona Arobaini yake
imefika ,wananchi wamemkamata na ndio hivyo kama unavyoona kapigwa
sana"alisema Mbaruku.
Alisema mtu huyo alifanikiwa kuiingia katika banda la nguruwe na
kukikamata mmoja ya kitoto cha nguruwe ambacho wakati wa harakati ya
kuingizwa katika mfuko huo kilipiga kelele ambazo ziliwashitua
majirani wengine.
Kutokana na mazingira hayo,mtuhumiwa huyo alikuwa mjasiri na kukimbia
nacho hivyo hivyo jambo lililosababisha baadhi ya wananchi kuanza
kumfukuza kwa kasi ndipo alipoanguka eneo la mfoni ambapo wananchi
walimjeruhi kwa silaha hizo ikiwamo mawe.
Katika hali isiyo ya kawaida huku mtuhumiwa huyo akivuja damu nyingine
mmoja wa raia alitaka kumchoma kwa gurudumu la gari ndipo wananchi
wenzake walipoingilia kati na kumuokoa mtuhumuwa huyo ambaye
alipelekwa kituo cha polisi bomangombe.
Hadi kipindi hiki kinaondoka eneo la tukio majira ya saa saba mchana
mtuhumiwa huyo alikuwa hajitambui kutokana na kipigo hicho kutoka kwa
raia ambao baadaye walitawanyika baada ya kuhisi wamefanya mauaji.
Mkazi wa kijiji cha Nshara Machame akivuja damu baada ya kupokea
kipigo kutoka kwa wananchi wenye hasira kali kufuatia wizi wa mtoto wa
Nguruwe,tukio hilo lilitokea juzi wilayani Hai.Picha na Dixon
Busagaga wa Globu ya Jamii - Moshi.
ReplyDeleteTemingi imekataa babaangu, kitimoto katokea puani
Wachagga mnanifurahisha sana. Mtu akiiba kidogo anauawa lakini akiiba mabilioni anaitwa shujaa na kupewa shikamoo hata kama ni mtoto mdogo.
ReplyDeleteKama wizi ni mila ya wachagga kwa nini walitaka kumuuwa mwenzao? Au kwa vile haibi vitu vikubwa? Kumbukeni roma haikujengwa kwa siku moja.
ReplyDeleteAisee babangu mmemuonea huyo mangi. Kwani wisi si ni mila yetu?
ReplyDeleteMungu awasamehe awajui walitendalo
ReplyDeleteMekuu ,mbe aithee tufanye mpango ingine bwashee!
ReplyDelete...(chalii ya nguruwe/ mtoto wa nguruwe) a.k.a kitoweo ya Krismasi imeota mbawa!
...Mimi nachukua nguruwe toto moja tu napigwa, ningeiba pesa mbee?
ReplyDeleteAhhh mwanawane, Krismasi 'dume' Mujini Moshi !!!
ReplyDeleteMimi Mangi kitoweo cha Krismasi kimeniponza, si afathali masee ningekula kabechi?
ReplyDeleteMekuu ngalasoni eeeh,
ReplyDeleteNinge iba kwa waswahilii ningekufwaa , sasa naiba kwa sisi mnaniuwaa?
Kisusio ya Krisimasi nungetengeneza na ninie?, na maji ya kisimanii au damu ya panyaa?
Naulisa mie Mekuu.
Nimeiba kitoto cha nguruwe kipondo kama hiki !!!
ReplyDeleteje,ningeiba Bilioni 1 si nisingeiona Krisimasi ningekuwa tayari Kaburini?
Mimi naiba nguruwe mchanga mdogooo Wachagga wenzangu mnanipiga kama hamnijui kabisa hapa Kijijini Moshi!
ReplyDeleteJe, ningeliiba huko Manzese Dare salaaam kwa Waswahili si ningeuliwa eeeh?
Ofisi ya Serikali za Mitaa ya Chama cha Siasa Kinachotawala Moshi, haya yanafanyika mpo?
ReplyDeleteItikadi yenu ni ya jazba na mapanga mkononi, mngechelewa mngemkuta jamaa Mangi akiwa amekatwa kawoshi masikio, mikono na viungo vingine kwa mapanga na visu !
Kisa?, nguruwe mmoja mtoto!