Na Mwandishi wetu

UONGOZI wa klabu ya Mtibwa Sugar umeiwekea ngumu klabu ya Yanga kuhusiana na ombi la kurudishwa kipa wake, Shaaban Kado kwenye timu hiyo au kusajiliwa na timu ya Coastal Union.

Mratibu wa timu hiyo, Jamal Bayser alisema kuwa walipokea barua kutoka Yanga ikiwataka kumrejesha kipa wao huyo kwa vile amesajili kwa mkopo na wao kuweka ngumu kutokana na makubaliano yao kuhusiana na kipa huyo.

Bayser alisema kuwa wao walikubaliana na Yanga kumchukua Kado kwa msimu mmoja, na kushangazwa na hatua ya klabu hiyo ambayo ilibadili msimamo wake hasa baada ya kipa wao, Yaw Berko kutolewa kwa mkopo.

Alisema kuwa Yanga pia iliwataarifu kuhusiana na mpango wao wa kutaka kumpeleka Kado Coastal Union, lakini ikashindikana tena kwa kipengele kile kile cha mktaba wa awali.

“Kado atacheza Mtibwa Sugar mpaka mwisho wa msimu kama ilivyokuwa makubaliano yetu, hivyo hawezi kurejeaYanga wala kwenda Coastal Union,” alisema Bayser ambaye ameongeza nguvu timu yake kwa kumsajili mchezaji wa zamani wa Vital’O ya Burundi, Stanley Minzi na kumpandisha kinda wao, Rajab Zahir.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...