Ubao wa matangazo ukionyesha namna ambavyo kila Nchi ilivyopiga Kura yake Azimio Kuhusu hali ya Syria, upigaji kura huo ulifanyika wakati Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa lilipokutana siku ya Jumatano. Azimio hilo lilipitishwa kwa kura za ndiyo 107, za hapana 12 na 59 za kutofungamana na upande wowote. Madhumuni ya Azimio hilo ni kuchagiza usitishaji wa mapigano ya wenyewe kwa wenyewe yanayoendelea nchi humo. Ingawa Azimio hilo limepita lakini limelalamikiwa kwamba mchakato wake haukuwa wazi, shirikishi, halikuzingatia ushauri wa wajumbe wengine na lilikuwa limeegema upande mmoja.
Home
Unlabelled
UMOJA WA MATAIFA WAJARIBU TENA KUISAIDIA SYRIA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...