Ewe mshabiki wa muziki wa dansi wa hapa nyumbani uliotamba katika miaka ya sabini hadi tisini, usikose kujivinjari katika ukumbi wa maraha wa nyumbani lounge kila siku ya jumatano kuanzia saaa tatu usiku, ambapo Isaac Muyenjwa Gamba akishirikiana na mchambuzi wa muziki wa dansi Rajabu Zomboko, watakuletea disco la muziki huo pamoja na miondoko ya bakulutu, katika BAKULUTU NITE ndani ya nyumbani lounge.

Njoo wewe na yule upate zile za Dar International, maquiz du zaire, ochestra safari sound, sikinde ngoma ya ukae , msondo ngoma nk, bila kusahau za francoo luambo makiadi, tabuley, sam mangwana na bibie mbilia bell live ambazo hazijachakachuliwa. Pichani Isaac Muyenjwa Gamba akiwa mitamboni ndani ya club ya numbani lounge akiwapagawisha vijana wa zamani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 06, 2013

    Fanya siku ya wikiendi tutakuja wengi. Usisahau akina Veve, Lipua Lipua, Les Kamalee n.k

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...