Mshauri wa Radio Jamii kutoka UNESCO Rose Haji
Mwalimu akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Karagwe Dary Lwegasira
alipomtembelea ofisini kwake mjini Kayanga mkoani Kagera kutambulisha
mradi wa Amani na Demokrasia wenye lengo la kuhamasisha ushiriki wa
jamii miongoni mwa vijana, wanawake na walemavu katika maendeleo na
kudumisha amani nchini Tanzania. Mradi huo utakuwa unaratibiwa na
UNESCO kwa kushirikiana na UNDP.
Mweka hazina wa Shirikisho la Vijana la Umoja wa
Mataifa (YUNA) Tanzania Bara na Visiwani Bw. Omary Hassan akifafanua
jambo kuhusiana na mradi wa Amani kwa Mkuu wa Wilaya ya Karagwe Dary
Lwegasira (wa tatu kulia) namna utakavyoendeshwa kwa wakazi wa Wilaya
yake. Kushoto ni Mkurugenzi wa Radio jamii FADECO ya Wilaya ya
Karagwe Joseph Sekiku na wa pili kulia ni Mshauri wa Radio Jamii
kutoka UNESCO Rose Haji Mwalimu.
Picha juu na chini ni Bw. Omary Hassan
akikusanya maoni ya vijana wa Chuo cha Ufundi Stadi (KDVTC) kilichopo
kitongoji cha Kayanza wilayani Karagwe mkoa wa
Kagera. picha zaidi bofya hapa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...