Kamishina Msaidizi wa Madini, (Leseni), John Nayopa na wajumbe alioongozana nao kutoka  Ofisi ya Madini Kanda ya Kusini- Magharibi  na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Chunya wakiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Mafunzo kwa wachimbaji wadogo cha Katundasi wilayani Chunya, Injinia Paul Gongo (wa pili toka kushoto) mara baada ya kumaliza ziara ya kutembelea kituo hicho kwa ajili ya kupata taarifa ya mafunzo kwa wachimbaji wadogo yanayoendeshwa na kituo hicho.
Serikali imesema kuwa itahakikisha inaendelea kutoa fursa za mafunzo kwa wachimbaji wadogo nchini ili wapate utaalam utakaowawezesha kufanya shughuli za uchimbaji madini kwa tija.
Hayo yamesemwa na Kamishina Msaidizi anayeshughulia Leseni  katika Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi John Nayopa, katika Kituo cha Mafunzo kwa Vitendo cha Matundasi wilayani Chunya ambacho hutoa mafunzo ya uchimbaji na uchenjuaji wa dhahabu kwa wachimbaji wadogo.

Mhandisi John Nayopa aliusisitiza uongozi wa kituo hicho kuhakikisha wanajitangaza kwa umma ili watu wenye uhitaji wa mafunzo waweze kufika kituoni hapo na kupata huduma zao kwani lengo la Wizara ya Nishati na Madini na Serikali ni kuhakikisha elimu kuhusu madini inawafikia wanachi wengi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...