Adubo Mustafa Omer Enzi ya uhai wake

Picha hapo juu ndiye marehemu Adudo Omer ambaye maiti yake ipo montuary Dallas Texas nchini Marekani tangia Aug 26, 2013 bado wanatafutwa ndugu, jamaa au watu wanaomfahamu marehemu popote pale walipo. Marehemu alizaliwa April 25, 1956.

Marehemu alishawahi kuishi kwenye miji ifuatayo hapa Marekani  Lincoln na Omaha miji iliyopo Nebraska. pia alishawahiishi Des Moines naCedar Rapids miji iliyopo Iowa.

Tafadhali tunaomba ndugu au mtu yeyote anayemfahamu  marehemu wajitokeze

Tafadhali wasiliana na 
Ben Kazora@ 269 873 0937
Viola Mbise @ 405 613 3445
Frank Maji@ 214 674 6666

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. Ni kabila gani?na kabla ya kukimbilia uko alikuwa anafanya kazi wapi?kwa hapa tanzania kwa kuanzia hapo tutamtafuta nakupata ndugu

    ReplyDelete
  2. Tatizo ni pale Mtanzania anapokuwa amejiita mkimbizi kutoka Burundi au Sudan; na ukakuta hajawahi kurudi home miaka zaidi ya ishirini. Ikiwa aliondoka kijana akiitwa Robert Mjuni wa Bukoba, na baadaye akabadili uraia na majina kinyemela na kuitwa Adubo Mstafa Omer, ni vigumu kwa ndugu zake kumtambua. Mdau Sweden.

    ReplyDelete
  3. Tafadhali tuwe wastaarabu watoa maoni hasa kwa jambo la kifo. Tumeshaonyeshwa sura yake. Tusiulize tena ADUBO ni jina la Nigeria au Burundi. Hii yote ni kutafuta maisha. WAHUSIKA WANAOMJUA WAJITOKEZE NA WASEME KAMA HUYU TUNAMJUA NA JINA LAKE HALISI NI RWEGOSHORA AU ROBERT MUJUNI N.K ILI ASITIRIWE VIZURI NDUGU YAO NA ASIZIKWE KAMA MNYAMA.

    ReplyDelete
  4. Poleni sana kwa msiba.
    Tunamuombea kwa mungu ndugu waweze kupatikana kwa haraka kwani kila mja wake anahaki ya kuzikwa kwa heshma zote.
    Roho ya marehemu ipunzike mahali pema peponi. Amen

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...