HATIMAYE ile siku iliyokuwa inasubiriwa na wengi, imewadia, ni GURUMO 53 ndani ya viwanja vya TCC Club, Chang’ombe leo Jumamosi Disemba 14.

Kama tangazo linavyojionyesha, ni tamasha kubwa la muziki wa dansi la kustaafu kwa gwiji Muhidin Maalim Gurumo aliyeitumikia fani hiyo kwa miaka 53 mfululizo. Gurumo ataimba angalau wimbo mmoja au zaidi wa kila bendi aliyopitia katika safari yake ndefu kimuziki.

Hadi kustaafu kwake Gurumo aliyezitumikia pia bendi za Kilimanjaro Chacha, Rufiji Jazz, Kilwa Jazz, Sikinde na OSS – Ndekule, alikuwa ni kiongozi na mmoja wa wamiliki wa Msondo Ngoma ambayo hapo awali ilijulikana kwa majina ya NUTTA, Juwata na OTTU. Gurumo ameitumika Msondo katika majina yote ya nyuma.

Ama kwa hakika ni burudani ya kukata na shoka, bendi kibao, wasanii kibao – ni burudani mwanzo mwisho kuanzia saa 12 jioni mpaka majogoo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...