Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Mizengo Pinda (kulia) akikata utepe kuzindua ripoti ya hali ya Uwekezaji nchini Tanzania leo jijini Dar es salaam. Pamoja na mambo mengine ripoti hiyo imegusia sera na na maendeleo ya uwekezaji nchini pamoja na changamoto zinazokwamisha ustawi wa uwekezaji Tanzania.
Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda akionyesha vitabu vya ripoti ya Uwekezaji Tanzania kwa wadau mbalimbali waliohudhuria uzinduzi wa ripoti kuhusu hali ya Uwekezaji nchini Tanzania leo jijini Dar es salaam.
Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda akimkabidhi kitabu cha Ripoti ya hali Uwekezaji nchini Tanzania Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Dkt. Reginald Mengi (kulia) leo jijini Dar es salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...