Mkurugenzi wa Masoko na Maendeleo ya Biashara wa Benki ya Posta Bw. Deo Kwiyukwa (wa pili kulia) akitoa maelekezo kwa baadhi ya viongozi na wanachama wa Simba waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa kadi za akaunti za benki hiyo kwa ajili ya wanachama na mashabiki wa vilabu vya Simba na Yanga leo katika hoteli ya Hyatt Kilimanjaro jijini Dar es salaam
 Mkurugenzi wa Masoko na Maendeleo ya Biashara wa Benki ya Posta Bw. Deo Kwiyukwa akimkabidhi mtangazaji Ephraim Kibonde wa Clouds FM mfano wa kadi ya akaunti ya benki hiyo hafla ya uzinduzi wa kadi za akaunti za benki hiyo kwa ajili ya wanachama na mashabiki wa vilabu vya Simba na Yanga leo katika hoteli ya Hyatt Kilimanjaro jijini Dar es salaam. Kushoto ni msemaji wa Simba Bi Asha Muhaji na kulia ni Afisa habari wa wekundu hao wa Msimbazi Bw. Kamwaga
  Mkurugenzi wa Masoko na Maendeleo ya Biashara wa Benki ya Posta Bw. Deo Kwiyukwa akimkabidhi mmoja wa mashabiki wa Yanga  kadi ya akaunti ya benki hiyo hafla ya uzinduzi wa kadi za akaunti za benki hiyo kwa ajili ya wanachama na mashabiki wa vilabu vya Simba na Yanga leo katika hoteli ya Hyatt Kilimanjaro jijini Dar es salaam. Kushoto ni msemaji wa Simba Bi Asha Muhaji na kulia ni Afisa habari wa wekundu hao wa Msimbazi Bw. Kamwaga
 Kadi ya akaunti ya Benki ya Posta kwa mwanachama wa Yanga, ambapo wao wameanza na wanachama kufungua akaunti na kupata kadi hii, na baada ya miezi mitatu mashabiki watafanya hivyo
  Kadi ya akaunti ya Benki ya Posta kwa mwanachama wa Simba. Tofauti na Yanga kadi za Simba zitaanza kugawiwa kwa mashabiki ambao watafungua akaunti, na baada ya miezi mitatu wanachama watapata fursa hiyo. Picha na Sultani Kipingo wa Globu ya Jamii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 30, 2014

    Je ni Vipi Kadi za Benki kwa Mabingwa Wapya wa Soka la Tanzania AZZAM ?

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 30, 2014

    Hahahahahah!

    Benki ya Posta wabunifu sana, wameelewa ktk Simba na Yanga ndipo pa kuwashika watu kirahisi.

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 30, 2014

    Mimi nitakata Rufaa Mahakamani kuweka pingamizi.

    Kwa kuwa hata hao Simba na Yanga wana Wababe wao ilibidi pia na Timu hizo za Vishoka wengine Mgambo JKT na JKT Ruvu pia wapewe Kadi za Benki, kama Mgambo JKT(Wababe wa Yanga) na JKT Ruvu(Wababe wa Simba)!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...