MAREHEMU AYOUB FELIX MLAY
Ni mwaka mmoja umepita tangu uhai wako ulipotolewa bila sababu na bila kutuaga na kutangulia kwenye pumziko la milele mbinguni. Unakumbukwa na Wazazi wako Felix na Amina Mlay wa Kiboriloni Moshi,watoto wako Erick,Dereck na Michelle,pamoja na Mama zao,Jane na Vicky.
Bila kuwasahau wadogo zako Adam,Gabriel,Charles,John,Richard na Dada zako wapendwa Sarah,Eunice,Neema,Diana,Ludie na Marafiki zako wote wa Moshi,Arusha na Dar es Salaam wakiwakilishwa na Ndugu Theoflo na Muheshimiwa Rita Mlaki na Wanachama wote wa RG Sports Club (Rose Garden Club) ya Dar es Salaam. Upole na ucheshi wako utakumbukwa daima na tunaanini siku moja tutakutana mbinguni. Upumzike kwa Amani.
inauma sana
ReplyDelete