Familia ya Marehemu Mzee Augustine Cassian Mwingira kutoka Mjimwema, Kigamboni inasikitika kutangaza kifo cha mpendwa wao, mzee Augustine Cassian Mwingira kilichotokea Jumanne, 27 Mei 2014 ktk Hospital ya Hindu Mandal alipolazwa baada ya kuugua kwa muda mfupi.
Msiba upo Nyumbani kwa Marehemu Mjimwema, Kigamboni "Kwa Mwingira". 
Ratiba ya Mazishi ni kama ifuatavyo;
Ijumaa, 30 Mei 2014
Saa 10 Jioni - Mwili wa Marehemu kuwasili Nyumbani kwake Maweni - Mjimwema, Kigamboni. 
saa  11 jioni - Misa/Ibada ya kumuombea marehemu itakayofanyika hapo hapo nyumbani
Saa 1 usiku - Chakula cha jioni
Baada ya hapo ni sala na maombi mbalimbali yataendelea

Jumamosi, 31 Mei 2014
Saa 4 Asubuhi - Misa Takatifu
Saa 5 Asubuhi - Chakula
Saa 6 Mchana - Heshima za mwisho kwa Marehemu
Saa 7 Mchana - Safari ya kuelekea Makaburi ya Kinondoni
Saa 8 Mchana - Shughuli za Mazishi kwenye Makaburi ya Kinondoni (Ndani)
Bwana alitoa na Bwana ametwaa, jina la Bwana lihimidiwe - Amen

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 30, 2014

    Alikuwa mkuu wa mkoa wa wapi vile?

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 30, 2014

    Arusha.Pia wazi wa mawasilina na uchukuzi

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 30, 2014

    Mkoa wa Mara na Arusha.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...