JAMHURI
YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA
UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO
MAMLAKA YA
VIWANJA VYA NDEGE TANZANIA
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu
imeipongezaSerikali kupitia Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) kwa
kujenga jengo zuri la tatu la abiria (TB III)
litakaloboresha zaidi huduma za usafiri wa anga.
Pongezi hizo zimetolewa na
Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Profesa Norman Sigalla (Makete) wakati Wajumbe wa
Kamati hiyo walipotembelea jengo hilo katika ziara yao ya kukagua miradi ya
Serikali mwanzoni mwa wiki.
Jengo hilo linajengwa katika
Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA) kwa Euro milioni 254
(sh. Bilioni 560) za mkopo kutoka Benki ya HSBC ya Uingereza na CRDB kwa
dhamana ya Serikali ya Tanzania na Uholanzi.
Tayari TAA imeshamlipa
Mkandarasi wake, Bam International ya Uholanzi, Euro milioni 96 baada ya
kukamilisha asilimia 60 ya kazi. Jengo hilo linajengwa kwa awamu mbili ambapo
awamu ya kwanza ipo katika hatua za mwisho.
Mwenyekiti Sigalla na Wajumbe
wengine wa Kamati hiyo walieleza kuridhishwa na kazi nzuri iliyofanywa na
Serikali kujenga jengo hilo linalotarajiwa kukamilika Desemba 2017.
Baada ya kufurahishwa na kazi
hiyo nzuri na kushauri uboreshaji zaidi wa utendaji, wabunge waliahidi
kuisukuma Serikali iiwezeshe zaidi TAA kifedha ikamilishe miradi yake kwa
wakati.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...