Pichani chini ni baadhi ya wananchi wakiweka masalia ya Kichwa cha Mtoto, Nasra Mkinze mwanafunzi wa Darasa la Pili, ambapo haikufahamika mara moja jina la shule hiyo, baada ya kugongwa na Gari la Mwendokasi T 953 DGV kwa kile kinacho daiwa chanzo ni Mwendesha Bodaboda MC 351 AWX kutaka kuwahi mataa ya Shekilango Dar es Salaam mchana huu  na ndipo Dereva huyo wa mwendokasi kuruhusiwa na kumgonga akiwa amembeba Shemeji yake na mtoto (akimwita baba mdogo) dereva wa Bodaboda walipokua wakienda mkoani Morogoro kwenye arobaini  . (PICHA NA KHAMISI MUSSA )
  Msamaria Mwema akiweka ndani ya Gari la Polisi mwili wa mtoto  Nasra Mkinze mwanafunzi wa Darasa la Pili,
 Wananchi wakiwa wamelizingira Gari la Mwendokasi.
  Askari wa Usalama Barabarani akizungumza na wananchi eneo la tukio na Pikipiki iliyosababisha ajali hiyo ikiwa imezungukwa

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 19, 2016

    Poleni wafiwa, kama ni alama za punguza mwendo au bumps kwenye maeneo ya vituo zinatakiwa maboresho yafanywe ili mwendo wa kasi usihatarishe maisha ya wengine..

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 19, 2016

    Poleni na msiba.
    Ila jamani kwani hakuna gari maalum za polisi kubeba maiti ? maana naona hii gari kama ya mizigo vile na ipo chafu.

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 19, 2016

    So very sad, RIP little angel.

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 19, 2016

    ikiwa taa inamruhusu dereva kupita na chombo chake haimaniishi kuwa asiwe mwangalifu na wenye kwenda kwa miguu au wenye vyombo vingine , ni wajibu wake kuhakikisha kuwa ni salama kabla kuondoa chombo chake. Mara nyingi tumeona ajali zikisababishwa na dereva kwa kuwa tu eti taa inamruhusu basi yeye hajali chochote hata kama kuna mtu au chombo mbele yeye hugonga tu kwa kutarajia sheria itamlinda kwa kuwa alipita wakati taa inamruhusu

    ReplyDelete
  5. Magari ya mwendo kasi yana barabara yake maalum kwa hiyo ukigongwa nalo inamaanisha wewe ndio umeingilia barabara yake ambayo imetengwa kwa ajili ya yale ma basi tu na sio chombo kingine chochote kile.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...